PROFESA CHIJORIGA AZUNGUMZIA CHACHU YA AMANI, UTULIVU NA MSHIKAMANO WA KITAIFA
Mkuu
wa Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere (MJNLS), Profesa Marcellina
Chijoriga, amesisitiza kuwa huu ni wakati muafaka kwa Watanzania kutafakari
misingi ya umoja na utulivu iliyowekwa tangu uhuru mwaka 1961 ili kuhakikisha
nchi inabaki kuwa salama kwa maendeleo ya wote.
Alisema
hayo katika kongamano wa kuadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa kwa Baba wa Taifa,
Hayati Julius Kambarage Nyerere, Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Dar es salaam leo.
Aliitaka
jamii kutumia kongamano hilo kukumbushia
maisha ya kiongozi huyo kama dira ya kudumisha amani na mshikamano wa kitaifa.
“Amani
na utulivu tulionao leo ni matokeo ya misingi imara ya uadilifu na uzalendo
ambayo Mwalimu Nyerere alisimamia kwa dhati wakati wa uongozi wake” alisema Profesa Chijoriga ambaye pia alibainisha kuwa
urithi huo si wa kihistoria pekee, bali ni wajibu wa kila Mtanzania wa kizazi
hiki kuuendeleza kwa vitendo.
Ili
kuendelea kuwa na taifa lenye mshikamano, alisema ni muhimu kuzingatia ulinzi
wa maadili ya kitaifa ambapo kila mwananchi anapaswa kuishi kwa kuzingatia
maono ya Baba wa Taifa yanayosisitiza uadilifu, haki, na uwajibikaji katika
kila nyanja ya maisha.
Aidha,
kudumisha umoja na utu ni msingi muhimu uliotujenga kama taifa linalojali
heshima ya kila mtu bila ubaguzi, jambo ambalo ni muhimu katika kuepuka
migogoro na kuimarisha utulivu wa ndani.
Vilevile,
alizungumzia uzalendo katika maendeleo na amani ya nchi inategemea ushiriki wa
dhati wa wananchi katika kujenga uchumi jumuishi, huku wakilinda rasilimali na
miundombinu ya kimkakati ambayo ni mali ya taifa zima.
Mshikamano
wa Watanzania ndio nguvu kuu, na kwa kumtazama Mwalimu Nyerere kama kielelezo
cha uongozi unaojali utu na haki za binadamu kutasaidia kuvuka changamoto za
sasa na kulifanya taifa kuendelea kuwa kimbilio la amani na utulivu barani
Afrika na duniani kote.

Post a Comment