HABARI MAALUM: Jeuri ya Tanzania na vita vya kiuchumi vya Tanzania



Matukio yaliyovuta hisia za dunia hivi karibuni nchini Tanzania si matukio ya pekee. Bali ni mlipuko wa vita ya miaka minane (2017–2025) ya kijiografia-kisiasa na kiuchumi, iliyoanza pale taifa hili lilipothubutu kuandika upya sheria za umiliki wa rasilimali.

 

♟️ Ubao wa Kimataifa wa Kuchezea Sataranji (chesi)

Tanzania haikabiliwi tu na mgogoro wa ndani, bali inajikuta imenaswa katika vita ya kiuchumi-kijiografia (geo-economic war) ya hatari kubwa ambayo imekuwa ikifunuka kama mchezo kwenye ubao wa kimataifa wa kuchezea sataranji tangu mwaka 2017. Vita hii haipiganwi kwa silaha za kawaida, bali kwa shinikizo la kiuchumi, mikakati ya kidiplomasia, na vita iliyoratibiwa ya kidijitali.

Mivutano ya sasa, iliyofikia kilele chake katika matukio ya Oktoba 29, 2025, ni mlipuko wa shinikizo lililojengeka kwa miaka kadhaa (2017,  2021 ,2023 , 2025).

⚖️ Mabadiliko Yasiyotarajiwa ya Mwaka 2017

Chanzo cha mgogoro huu kiko mwaka 2017, mwaka ambao Tanzania ilitekeleza kile kilichoitwa "kisichowezekana" ("the unthinkable"). Bunge lilipitisha sheria mbili za kimapinduzi ambazo kimsingi ziliipinga sekta ya uchimbaji wa madini duniani:

  • Sheria ya Umiliki wa Kudumu wa Rasilimali Asilia (2017).
  • Sheria ya Mapitio na Majadiliano Upya ya Mikataba ya Rasilimali Asilia (2017).

Kimsingi, sheria hizi zilitangaza kwa ulimwengu: "Madini yetu. Masharti yetu. Uhuru wetu. Nukta." Hatua hii ilionyesha kwa kampuni kubwa za uchimbaji kuwa Tanzania haikuwa tena "uwanja wa kuchezea" waliouzoea, ikisisitiza kuwa kampuni za kigeni zingefanya kazi chini ya "sheria mpya. Sheria zetu."

Rais Magufuli aliita waziwazi msimamo huu wa kisera kama "Vita ya Kiuchumi," akisisitiza kuwa nchi ilikuwa imeingia kwenye uwanja wa vita ikipambanisha madini dhidi ya mataifa makubwa, na uhuru dhidi ya tawala za zamani.

🌪️ Kisasi na Simulizi Mbadala

Kisasi kilikuwa cha haraka. Kwanza, ilianza kuzinduliwa simulizi mbadala ya haraka katika anga za kimataifa. Wakati masuala kadhaa ya ndani yalikuwepo, simulizi iliyodai kuwa "Tanzania inafuata mfumo wa kiimla," "Uhuru wa vyombo vya habari unapungua," na "Upinzani unapungua"—pia ilikuwa ni shinikizo kubwa la kimataifa. Ujumbe katika hili ulikuwa wazi: huwezi kuandika upya mikataba ya rasilimali yenye thamani ya mabilioni bila kukabiliwa na kisasi cha mabeberu wawekezaji hawa.

🤝 Utulivu Kabla ya Dhoruba (2021)

Kufuatia mpito wa uongozi mwaka 2021, Rais mpya alichukua msimamo mtulivu zaidi, ulioambatana na tabasamu la kidiplomasia, kupeana mikono, na kukumbatiana. Serikali za Magharibi hapo awali ziliamini dhoruba ilikuwa imepita. Hata hivyo, utulivu huu wa kidiplomasia waliouona ulikuwa wa kupotosha kwani aliyeingia pamoja na utulivu waliouna aliendelea na mpango wa taifa.

Miradi miwili ya kimkakati ya rasilimali ilikuwa ikijenga hatma ya muda mrefu ya Tanzania, hatimaye kupandisha sana joto la kimataifa:

  • Mkuju Uranium.
  • Lindi LNG.

☢️ Sumu ya Uranium: Urusi Yaingia Kwenye Kinyang'anyiro

Mradi wa uranium wa Mkuju si tu operesheni nyingine ya uchimbaji; una moja ya akiba kubwa na muhimu ya kimkakati za uranium duniani. Katika mazungumzo mengi , mradi huo haukupewa mataifa ya Magharibi kama Marekani au Ufaransa, bali ulipewa Rosatom, shirika la Serikali ya Urusi linaloshughulikia masuala ya nyuklia.

Mshangao wa kisiasa ulizidi mnamo Julai 31, 2025, wakati Tanzania na Urusi zilipozindua rasmi kiwanda cha majaribio cha kusindika uranium pale Mkuju. Kwa upande wa Mataifa ya  Magharibi, hii haikuonekana kama biashara tu, bali kama tishio la kiusalama, ikizingatiwa kuwa uranium inahusiana na uwezo wa nyuklia, wakaona kuwa Urusi sasa inaidhibiti akiba ya uranium iliyopo ambayo Tanzania ipo nafasi 10 za juu duniani.

Bomu la Pili: Gesi na Kuelekea Mashariki

Suala kuu la pili la mzozo lilikuwa mradi wa Lindi wa gesi LNG. Makampuni makubwa ya Magharibi (Shell, Equinor, ExxonMobil, n.k.) yalikaa miaka mingi kujadili mkataba kuhusu gesi hii (2018–2023) bila mafanikio. Hata hivyo, hali ilibadilika ghafla wakati maslahi yalipoibuka baada ya mataifa ya Mashariki na Ghuba, yaani China, Mataifa ya Ghuba, na Gazprom ya Urusi vikionesha nia ya kuingia katika mradi huo mkubwa wa gesi.

Sasa unauona mnyororo huo—Uranium inaenda Urusi; Gesi inaenda China/Ghuba/Urusi; kwa hiyo Diplomasia sasa inaelekea Kuegemea Mashariki na maana yake ni dhahiri kwamba msingi wa uhuru wa rasilimali ulioanzishwa mwaka 2017 ulibaki imara. Hii ilifanya ifikiri upya: " Hee kumbe hakuna kilichobadilika tangu 2017?"

📱 Uwanja wa Vita wa Kidijitali

Kwa kuona mbinu za jadi za kubanana kiuchumi zinakosa nguvu, mgogoro waliuhamisha kwenye uwanja wa vita vya kidijitali, ambapo vita vya kisasa hupigwa kwa usambazaji wa taarifa potofu, huku matumizi yakiwa ni alama za reli (hashtags), "bots," na simulizi zilizolipiwa ili kuleta mtafaruku.

Tanzania inaumizwa hapa kwani imetoa uwanja kamili wa vita kwa operesheni za kisaikolojia kutokana na udhaifu wa ndani katika nyanja tatu:

  • Idadi kubwa ya vijana waliokata tamaa.
  • Kizazi cha siasa kinachotegemea 100% mtandao.
  • Vikundi vya ndani vya kisiasa vyenye njaa ya kupata faida.

Kuanzia 2023 kuendelea, joto la mtandaoni lilipanda haraka isivyo kawaida, likichochewa na ajenda mbalimbali, kauli za kidini zikipata uzito wa kisiasa, na mgawanyiko wa kila siku.

Kipindi chote presha ilikuwa kubwa lakini Tangazo la Mkuju la Julai 31, 2025, lilitumika kama tamko thabiti, kubwa, na la kiishara kuhusu mwelekeo mpya wa Tanzania. Miezi mitatu baadaye, mnamo Oktoba 29, valvu ya shikizo la ‘jiko’  na kulipuka.

Tukio la Oktoba 29 halikuwa "la bahati mbaya" au "la ghafla"; ilikuwa ni mtririrko wa mambo katika miaka minane ya mvutano wa kisiasa. Tanzania, badala ya kuwa katika mgogoro rahisi wa ndani, inasalia kuwa kipande muhimu kwenye ubao wa kimataifa wa kuchezea chesi, watu wanataka madini kwa bei ya kutupa wao ndio wawe wadhibiti.


No comments