Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, September 5, 2013

GARETH BALE KUKUTANA NA VIZUIZI KAMA ALIVYOKUWA NAVYO OZIL, HAJAHAKIKISHIWA NAMBA YA KUDUMU KATIKA KIKOSI CHA KWANZA REAL MADRID!


Jembe jipya la Real Madrid Gareth Bale
Mchezaji mpya wa Real Madrid Gareth Bale hajahakikishiwa moja kwa moja kuwa atakuwa muda akianza katika kikosi cha kwanza pamoja na yeye kuwa mchezaji mwenye thamani kubwa kuliko wote baada ya kununuliwa hivi karibuni na klabu hiyo.

Kocha msaidizi wa Real Madrid Paul Clement amesema kuwa Gareth Bale licha ya kununuliwa kwa gharama kubwa ya zaidi ya paundi mili0ni 85 haimanishi kuwa kila mara atakua akianza katika kikosi cha kwanza.

Paul Clement amesema kuwa ndani ya klabu hiyo kuna ushindani mkubwa hivyo Gareth Bale pamoja nawachezaji wengine hawawezi wakahakikishiwa namba kulingana na hali halisi.
Kocha huyo msaidizi amesema kuwa mambo yatakuwa yakibadilika kulingana na mahitaji ya wakati huo na kwa namna kocha mkuu ataona inafaa.

Paul Clement ameongeza kusema kuwa kocha mkuu wa Real Madrid Carlo Ancelotti anafahamu namna ambavyo atamtumia mchezaji Gareth Bale lakini si lazima awe na namba ya kudumu katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo.



GARETH BALE vs CRISTIANO RONALDO
Kusajiliwa kwa mchezaji huyo kunamfanya aungane na straika bora kabisa wa Madrid, Cristiano Ronaldo, katika kusukuma mashambulizi ya timu hiyo.

Hali hiyo itaifanya timu hiyo kuwa na muungano hatari zaidi kwenye safu ya ushambuliaji, kutokana na wawili hao kuwa na rekodi zinazokaribiana.
GARETH BALE
Namba ya jezi: 11
Nafasi: Kiungo mshambuliaji
Umri: Miaka 24
Kuzaliwa: Julai 16, 1989
Alikozaliwa: Cardiff, Wales
Urefu: Futi 6 inchi 1 (1.83m)
Uzito: Kilo 74


CRISTIANO RONALDO
Namba ya jezi: 7
Nafasi: Mshambuliaji
Umri: Miaka 28
Kuzaliwa: Februari 5, 1985
Alikozaliwa: Madeira, Ureno
Urefu: Futi 6 inchi 1 (1.85m)
Uzito: Kilo 75

MSIMU ULIOPITA
MECHI WALIZOCHEZA

>Ronaldo 30
>Bale 34


MAGOLI
>Ronaldo 34
>Bale 21 


MASHUTI GOLINI

-Ronaldo 235
-Bale 165

MASHUTI YALIYOLENGA

-Ronaldo 105
-Bale 73
PASI ZA MABAO

-Ronaldo 10
-Bale 4
RAFU WALIZOCHEZA

-Ronaldo 27
-Bale 24
RAFU WALIZOCHEZEWA

-Ronaldo 81
-Bale 47

KADI ZA NJANO

Ronaldo 9
Bale 6
KADI NYEKUNDU

-Ronaldo 0
-Bale 0

THAMANI ZAO
GARETH BALE
Bale alihamia Spurs kutoka Southampton mwaka 2007 kwa kitita cha Pauni milioni 5 tu, inasemekana anatua Madrid kwa Pauni milioni 78.

CRISTIANO RONALDO

Alitua Manchester United akitokea Sporting Lisbon ya Ureno kwa kitita cha Pauni milioni 12.5 mwaka 2003 na kisha akatua Madrid kwa Pauni milioni 80.
(Hii inamaanisha kuwa ungeweza kuwanunua akina Bale 16 kwa bei ya Ronaldo wakati ule)

GARETH BALE

Kwa kutazama nje, nyota huyo wa Tottenham Hotspur, anaonekana kwamba ataweza kufiti katika mfumo wa Real Madrid kama atakuwa mchezaji wa klabu hiyo.


Winga huyo wa Wales, aina ya soka lake linafanana na la Ronaldo kwa kiasi fulani, kwa maana ya kasi, nguvu na chenga za aina yake.
Alichukuliwa na Spurs kutoka katika klabu ya Southampton kwa kitita cha Pauni milioni 5 tu mwaka 2007. Kipindi hicho, mchezaji huyo ndani ya kikosi cha Spurs ameweza kupandisha kiwango chake cha soka na kuwa moja ya mastaa wanaotetemesha soko la usajili kwa kipindi hiki.

Kwa aina ya uchezaji wake wa sasa, akiwa chini ya kocha Andre Villas-Boas, Bale ameweza kuonyesha kwamba ni tishio kubwa anapocheza kama mshambuliaji wa kati.
Uwepo wake kwenye kikosi cha Spurs, ambacho safu yake ya ushambuliaji imekuwa ikibadilika, lakini kuwapo kwa mchezaji huyo kumeifanya timu hiyo ya Ligi Kuu England kuwa na makali ya aina yake.
Kama ilivyo kwa Ronaldo, Bale ni mchezaji wa muda mrefu, kwamba unaweza kuwekeza kupitia yeye na ukawa kwenye mipango kwa muda mrefu zaidi.
Uwezo wake wa umaliziaji ni wa aina yake na kuhesabiwa kuwa mmoja wa washambuliaji ulimwenguni, huku anamiliki pia kiwango kikubwa cha uchezeshaji, kitu ambacho kinaweza kumpa nafasi ya kucheza katika klabu yoyote. Je, atafiti kwenye mfumo wa Madrid?

RONALDO
Ni straika wa aina yake, ambaye ni gumzo ulimwenguni.
Kumekuwa na imani kwamba Mreno huyo anatumia uvumi uliopo kwamba alitaka kurudi United ili kuifanya Real Madrid kutoa fedha nyingi kumbakiza, lakini ukweli halisi mchezaji huyo alifanikiwa kuishawishi Madrid ikamwongezea mkataba mnono.
Ronaldo si mchezaji tofauti sana na yule aliyehama United mwaka 2009, kwa sasa amezidi ubora wake zaidi. Kama Bale atapangwa naye, hakuna shaka kwamba ataendelea kutumika kama winga, ambayo ni nafasi yake ya asili.


Ni wazi kabisa kocha wa Madrid anaweza kufanya mabadiliko ya namba kwa ajili ya kukiweka sawa kikosi chake. Ronaldo atapewa nafasi pia ya kuzunguka uwanja mzima kutafuta mipira. Na kwenye hilo, Madrid haitaweza kutumia mfumo wa 4-2-3-1 kwa sababu jambo hilo litaacha nafasi kwenye kikosi, hasa kwa upande wa wachezaji wa pembeni.

No comments:

Post a Comment