Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, September 7, 2013

ENGLAND YAIFUNGA MOLDOVA 4-0 KATIKA MICHEZO WA KOMBE LA DUNIAMOLDOVA


Timu ya England ikicheza Uwanjani Wembley leo imeifunga timu ya Moldova bao 4-0, kwenye mechi yao muhimu ya Kundi H la Kombe la Dunia dhidi ya Moldova na Straika wa Southampton Rickie Lambert akitangulizwa kucheza mchezo huu kama mshambuliaji, Bao la kwanza la England limefungwa na timu kapteini Steven Gerrard katika dakika ya 12, Rickie Lambert akifunga bao la pili dakika ya 26.
Steven Gerrard akishangilia baada ya kufungua kwa kufunga bao la kwanza dakika ya 12 ya mchezo usiku huu.
Mchezaji matata wa manchester United Danny Welbeck akifunga bao mbili peke yake dakika ya mwishoni dakika za nyongeza za kipindi cha kwanza za dakika 45 na bao la pili akilifunga dakika ya 50 baada ya kupewa basi safi iliyotoka nyuma kwa Steven Gerrard na kupokelewa na mchezaji mwingine aliyemtangulizia kwa mbele Welbeck na hatimaye kutofanya makosa na kuipatia bao hilo la nne na kufanya England kuwa mbele ya bao 4-0 dhidi ya Moldova.  Lambert, akicheza Mechi yake ya kwanza tu ya England, Mwezi uliopita alitoka Benchi na kuifungia Bao la ushindi England ilipoifunga Scotland na leo hii ameifungia bao tena England la pili. Pamoja na Danny Welbeck kufunga bao mbili wenda akakosa mechi ijayo na Ukaine kwa kuwa mchezo huu ameoneshwa kadi nyekundu katika dakika ya 45 na refa wa mchezo huo.
 
Baada ya Mechi hii, England watasafiri kwenda Kiev ambapo Jumanne watacheza na Ukraine.  Steven Gerrard akiachia shuti kali na kufunga bao la kwanza Akishangilia hapaBao....mpira ukiishilia kwenye kambaAshley Cole kwenye anga zake Danny Welbeck akikacha na mpira kwenda kufunga bao la tatu Danny Welbeck akifunga bao lake la pili dakika za mwisho kipindi cha kwanza.
Welbeck akikacha baada ya kuziona nyavu tena!! akifunga bao la pili dhidi ya Moldova kwenye uwanja wa Wembley, LondonSteven Gerrard kwenye patashikaNipishe nipite!!


KUMBUKA TIMU HIZI ZILISHAKUTANA USO KWA USO
-Septemba 1996 Moldova 0 England 3 (Chisinau, Moldova)
-Septemba 1997 England 4 Moldova 0 (Wembley, London)
-Septemba 2012 Moldova 0 England 5 (Chisinau, Moldova)
-Septemba 2013 England 4 Moldova 0 ( Wembley, London)

RATIBA/MATOKEO
Ijumaa Septemba 6
England 4 v Moldova 0
Poland  1 v Montenegro 1
Ukraine 9 v San Marino 0
Jumanne Septemba 10
San Marino v Poland
Ukraine v England
Ijumaa Oktoba 11
England v Montenegro
Moldova v San Marino
Ukraine v Poland
Jumanne Oktoba 15
England v Poland
Montenegro v Moldova
San Marino v Ukraine

No comments:

Post a Comment