Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, September 6, 2013

CHEKI VURUGU ZA JANA BUNGENI

Wabunge wa Chadema wakiwa wamesimama kukaidi amri ya Naibu spika, Job Ndugai ya kuwataka wakae chini

Wabunge wa CHADEMA wakipambana na Polisi, Bungeni Mjini Dodoma leo
Chanzo cha kutolewa kwa amri hiyo ni kutokana na Mbunge wa Hai Freeman Mbowe kusimama na kuanza kuzungumza pasipo kupewa ruhusa ili apinge uamuzi wa kura zilizopigwa na Wabunge ambapo Bunge lilipiga kura ya kuuondoa mjadala wa mswada wa katiba au ubaki ambapo wabunge 56 walisema mjadala huo uondolewe na Wabunge 159 walisema mjadala huo uendelee kwani ulishapita kwenye hatua mbalimbali.
Mara baada ya zoezi la upigaji kura kuisha Naibu Spika Job Ndugai aliendelea na utaratibu wa Bunge ambapo alimsimamisha Mhe. Mrema achangie mjadala na wakati huo huo Mhe. Mbowe naye alisimama kupinga uamuzi wa Naibu Spika na ndipo alipotoa amri kwa askari wa Bungeni wamtoe nje ya ukumbi wa Bunge na walifanikiwa kumtoa nje mara baada ya mvutano mkali kati ya Wabunge wa kambi ya upinzania dhidi ya polisi.


Mbunge wa Kuteuliwa na Mwenyekiti wa NCCR_MAGEUZI, James Mbatia akisahangaa kuona mapambano kati ya wabunge wa CHADEMA na Polisi Bungeni

Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi aakiwa ameng'ang'ania Migrophone ya sehemu ya Kuzungumzia wapinzani Bungeni wakati polisi walipokuwa wakimtoa Bungeni Mjini Dodoma leo



Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi aakiwa ameng'ang'ania Migrophone ya sehemu ya Kuzungumzia wapinzani Bungeni wakati polisi walipokuwa wakimtoa Bungeni Mjini Dodoma leo. hata hivyo Microphone hiyo iling'oka na polisi wakafaikiwa kumtoa nje

Microphone hiyo iling'oka na polisi wakafanikiwa kumtoa nje
Patashika hapa!

Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi akitolewa na Askari Polisi nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma leo

Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe akiongoza wabunge wa CHADEMA kutoka Bungeni mjini Dododma baada ya kuamriwa kufanya hivyo na Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai


Mbunge wa Mbeya Mjini akizuiwa na wabunge wa CHADEMA ili asipambane na polisi, Bungeni Mjini Dodoma leo

Kwa hisani

No comments:

Post a Comment