SERIKALI YAELEZA SABABU YA UCHUMI IMARA
SERIKALI imesema Pato la Taifa kwa mwaka 2025 lilikua kwa wastani wa asilimia 5.9 ikilinganishwa na asilimia 5.5 mwaka 2024.
Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar alisema hayo
akiwasilisha Mapitio ya Utekelezaji na Mpango wa Bajeti kwa Mwaka wa Fedha
2025/2026 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027
bungeni Dodoma jana.
Balozi Omar alisema ukuaji huo ulichangiwa na kuongezeka kwa
mikopo kwa sekta binafsi, kuimarika kwa miundombinu ya usafiri na usafirishaji
na kuimarika kwa shughuli za kilimo. Alitaja sababu nyingine ni kutekelezwa
kama ulivyopitishwa na bunge.
Kuongezeka kwa uzalishaji wa madini na shughuli za ujenzi wa
umma na binafsi na utekelezaji wa miradi ya kimkakati, hususani katika sekta za
nishati, usafirishaji na huduma za jamii.
Balozi Omar alisema shughuli za fedha na bima ziliongoza kwa
ukuaji wa asilimia 15.7 ikifuatiwa na shughuli za uzalishaji na usambazaji
umeme na gesi 11.8%, uchimbaji madini na mawe 9.4%, habari na mawasiliano 8.8%,
sanaa na burudani 8.5% na usafirishaji na uhifadhi mizigo 8.0%.
Alieleza kuwa ukusanyaji wa mapato ya kodi umeen delea kuwa
zaidi ya asilimia 100 ya lengo la kila mwezi na mpango wa ukopaji kutoka vyanzo
vya kibiashara vya ndani na nje kuendelea Alisema hatua za kiutawa la na
maboresho ya mifumo ya kielektroniki ya usimamizi wa mapato zimewezesha Mamlaka
ya Mapato Tanzania (TRA) kukusanya mapato ghafi ya Sh trilioni 30.25, sawa na
ufanisi wa asilimia 105 ya lengo la kipindi cha rejea.
Alisema mapato halisi yaliyokusanywa na TRA ya likuwa Sh
trilioni 29.31 sawa na asilimia 86.0 ya lengo la mwaka na wizara ilikusanya
maduhuli ya Sh bilioni 25.5 sawa na ufanisi wa asilimia 47.6 ya lengo la mwaka.
Alisema kati ya Julai 2025 hadi Aprili mwaka huu mapato ya
ndani yaliyopati kana ni Sh trilioni 29.34 sawa na ufanisi wa asilimia 85.9 yalengo
la mwaka. Balozi Omar alisema kati ya kiasi hicho mapato ya forodha yalikuwa Sh
trilioni 11.49, kodi ya mapato Sh trilioni 10.95, kodi ya mlaji Sh trilioni
6.32, mapato yasiyo ya kodi Sh trilioni 1.22 na kodi nyingine Sh bilioni
266.72.
Alisema mwenendo wa viashiria vingine vya uchumi, katika
kipindi cha Julai 2025 hadi Aprili mwaka huu una onesha mfumuko wa bei uli kuwa
wastani wa asilimia 3.4, ikilinganishwa na wastani wa 3.1% katika kipindi kama
hicho mwaka 2024/2025.
“Ongezeko hilo lilito kana na kupungua kwa ugavi wa bidhaa
za vyakula katika soko la ndani kufuatia ongezeko la mauzo ka tika masoko ya
nchi jirani,” alisema. Balozi Omar alisema akiba ya fedha za kigeni ilikuwa
Dola za Marekani milioni 5,722.5, kiasi kinachotosheleza uagizaji wa bidhaa na
huduma kutoka nje ya nchi kwa kipindi kisichopungua miezi 4.4.
Alisema pia ilinunua tani 17.64 za dhahabu zenye thamani ya
Dola za Marekani milioni 2,616.77 na kufikisha tani 24.21 za akiba ya dha habu
zenye thamani ya Dola za Marekani milioni 3,591.39. Aidha, alisema hadi Aprili
mwaka huu taasisi zimechan gia Sh bilioni 341.53 katika Mfuko Mkuu wa Hazina ya
Serikali sawa na asilimia 79.95 ya lengo la mwaka.
Usimamizi deni Balozi Omar alisema Tanzania imeibuka mshindi
wa jumla katika Tuzo ya Usimamizi wa Deni la Umma katika nchi za Jumuiya ya
Madola na Tuzo ya Ofisi Bora ya Usimamizi wa Deni la Serikali katika Kanda ya
Afrika.
Alisema hadi Aprili mwaka huu Sh trilioni 9.73 sawa na
asilimia 68.5 ya lengo la mwaka zimepokele wa na kutumika kulipa deni la
serikali lililoiva. Kati ya kiasi hicho, Sh tri lioni 4.44 zimetumika kulipa
deni la nje na Sh trilioni 5.29 zimetumika kulipa deni la ndani. “Ufanisi
katika ulipaji deni lililoiva umeiwezesha nchi yetu kuendelea kuamini ka katika
masoko ya fedha ya kikanda na kimataifa,” alisema.

Post a Comment