RAIS SAMIA KUMALIZA ZIARA YAKE URUSI LEO

 


Na Beda Msimbe, TBN, St Petersburg                  

Rais Samia Suluhu Hassan leo anahitimisha ziara yake nchini Urusi kwa kushiriki katika kongamano la kibiashara kati ya Tanzania na Urusi sanjari na Jukwaa la Kimataifa la Biashara la St Petersburg.                    

Katika jukwaa hilo Rais Samia anatarajiwa kuinadi Tanzania katika sekta za uwekezaji na biashara.            

Ziara ya Rais Samia imekuwa na mafanikio makubwa hasa hakikisho la ushiriano wa karibu na Urusi katika nyanja mbalimbali ikiwemo elimu ya uendelezaji wa rasilimaliwatu na ukuzaji wa teknolojia. 

Ziara hiyo katika taifa lenye nguvu kubwa kiteknolojia, uchakataji na uzalishaji kwenye kilimo au viwandani imekuja wakati Tanzania inajiandaa kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050 inayolenga kulifanya taifa kuwa na pato la dola trilioni moja kwa mwaka.                      

Kwa sasa serikali imesema Pato la Taifa kwa mwaka 2025 lilikua kwa wastani wa asilimia 5.9 ikilinganishwa na asilimia 5.5 mwaka 2024 kauli ilitolewa na Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar wakati akiwasilisha Mapitio ya Utekelezaji na Mpango wa Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 bungeni Dodoma hivi karibuni.

 

Balozi Omar alisema ukuaji huo ulichangiwa na kuongezeka kwa mikopo kwa sekta binafsi, kuimarika kwa miundombinu ya usafiri na usafirishaji na kuimarika kwa shughuli za kilimo.

Alitaja sababu nyingine ni kuongezeka kwa uzalishaji wa madini na shughuli za ujenzi wa umma na binafsi na utekelezaji wa miradi ya kimkakati, hususani katika sekta za nishati, usafirishaji na huduma za jamii.

Mwisho Mwisho mwisho

No comments