UPANUZI WA BANDARI YA DAR ES SALAAM: GATI 10 MPYA NA MIUNDOMBINU YA UBARIDI KUWEZESHA USAFIRISHAJI WA MAZAO YA MBOGAMBOGA
Msemaji Mkuu
wa Serikali Gerson Msigwa , amesema Serikali imeanza
utekelezaji wa mradi mkubwa wa upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam
utakaogharimu dola za Marekani bilioni 2, sawa na zaidi ya shilingi trilioni 5.
Amesema
moja ya lengo la upanuzi huo ni kutatua changamoto za usafirishaji wa mazao ya
kilimo yanayoharibika haraka
Akizungumza
na waandishi wa habari mkoani hapa alisema Mradi huo unahusisha ujenzi wa gati
mpya 10 ili kufikisha jumla ya gati 22.
Aidha
kutakuwepo na ujenzi wa majengo ya ubaridi na miundombinu yake maalumu ili
kuondoa vikwazo vilivyokuwa vikiwakabili wakulima wa parachichi na mbogamboga
wakati wa kusafirisha bidhaa zao nje ya nchi
Kupitia
mradi huu, Serikali pia itaboresha barabara za kuingia na kutoka bandarini kwa
kujenga barabara za mzunguko ili kupunguza msongamano wa magari yanayobeba
mizigo, jambo litakalosaidia mazao kutoka mikoa ya uzalishaji kama Njombe
kufika bandarini kwa wakati na yakiwa na ubora uleule

Post a Comment