Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, March 10, 2015

TIMU YA SOKA BEACH KUIKABILI MISRI IJUMAA, ESCAPE 1






TIMU ya Taifa ya Tanzania ya soka la ufukweni (Beach Soccer) inatarajiwa kucheza na timu ya Taifa ya Misri  Machi 13 mwaka huu kwenye ufukwe wa Escape one Msasani jijini Dar es Salaam.

Mchezo huo wa raundi ya pili wa kutafuta kufuzu fainali za Afrika zitakazo fanyika visiwa vya Shelisheli utaanza majira saa 10 kamili jioni.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Afisa habari wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), Baraka Kizuguto, alisema  kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania kinaendelea na mazoezi kujiandaa ya mchezo huo, ambapo kwa takribani wiki mbili kipo kambini Bamba Beach wakijifua.

“Timu yetu ipo Kambini Bamba Beach ikiendelea na mazoezi kwa ajili ya mchezo na Misri kwani ni mchezo muhimu kushinda ili kufuzu kwa fainali za Afrika”, alisema Kizuguto

Tanzania ilifuzu hatua ya pili baada ya kuiondoa timu ya Taifa ya Kenya kwa jumla ya mabao 12 -9, na endapo itafanikiwa kuwaota Misri, itafuzu moja kwa moja kucheza Fainali za soka la Ufukweni zitakazofanyika Visiwa vya Shelisheli mwezi April  mwaka huu.

Pia alisema aamuzi wa mchezo huo ni Eid Haitham Eid Hassan toka Sudan, mwamuzi msaidzi namba moja ni  Abaker Mohamed Bilal wa Sudan pia.

Mwamuzi msaidizi namba mbili ni Abdalla Hassain Hassaballa, mtunza muda ni Boubaker Bessem wanatoka Tunisia, wakati kamisaa wa mchezo huo ni Khiba Herbert Mohoanyane kutoka Lesotho.

Mchezo wa marudiano unatarajiwa kufanyika wiki ijayo nchini Misri kati ya Machi 20,21 na 22 mwaka huu.

Timu ya Taifa ya Misri inatarajiwa kuwasili Dar es salaam leo mchana,na  itafikia katika hoteli ya Double Tree by Hilton iliyopo Masaki pia waamuzi wanatarajiwa kuwasili leo na watafikia katika hotel ya Protea Oysterbay.

Pia kesho makocha wa timu zote wataongea na vyombo vya habari katika ukumbi wa mikutano wa TFF uliopo Karume kuanzia majira ya saa 5 kamili asubuhi.

Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), inaitakia kila la kheri na ushindi timu ya Taifa ya soka la ufukweni (Beach Soccer) katika huo dhidi ya Misri.

No comments:

Post a Comment