Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, March 10, 2015

BODI YA LIGI YAAHIRISHA MECHI YA YANGA



TABIA ya Bodi ya Ligi kubadilisha ratiba imeendelea kuota mizizi ambapo jana imetangaza tena kuharishwa kwa michezo miwili ya Ligi Kuu Tanzania Bara ambayo iliyokuwa ichezwe leo.
Akizungumza na wandishi wa Habari, Afisa Habari wa Shirikisho la Soka Nchini, (TFF) Baraka Kizuguto alitangaza kuahirishwa kwa michezo ya JKT Ruvu dhidi ya Young Africans katika uwanja wa Taifa, na Mgambo Shooting dhidi ya Azam FC uwanja wa Mkwakwani jijini.
Kizuguto alisema michezo hiyo ambayo ilikuwa ichezwe leo sasa itapangiwa tarehe nyingine  bila kutoa sababu za kuhahirishwa.
Katika kutaka kusikia maoni ya wadau wa soka gazeti hili lilimtafuta meneja wa Azam FC Jemedariambaye alikuwa na haya ya kusema
 “Sisi tulikuwa tuondoke leo kwenda Tanga lakini cha kushangaza usiku tulipata taarifa toka BodI ya Ligi kuwa tusiende Tanga kwani mchezo huo umeharishwa na badala yake tujiandae na mchezo dhidi ya Ndanda FC ambao tutacheza jumamosi”, alisema Jemedari
Awali Yanga walilalamika mchezo huo dhidi ya JKT Ruvu kusogozwa mbele ambapo awali ulipangwa kuchezwa Machi 4, mwaka huu kudai watakosa muda wa kujiandaa na mchezo wa Kombe la Shirikisho ambao wanatarajia kucheza Machi 14 mwaka huu.
Wadau wa soka wamelalamikia kitendo cha ratiba ya ligi kupanguliwa kila mara ambapo hadi sasa imeshapanguliwa mara tatu bila sababu za msingi na kusema ratiba hiyo haieleweki zaidi inavuruga timu.

No comments:

Post a Comment