KING KIKII, MSONDO NGOMA NA KHADIJA KOPA JUKWAA MOJA SHEKINAH GARDEN.

Aidha Mwendapole amesema ili kuikamilisha burudani hii ya aina yake na inayofanyika kwa mara ya kwanza ndani ya Shekinah Garden mbezi makonde, malkia wa mipasho Afrika Mashariki na Kati Bi Khadija Omar Kopa naye atawakonga mashabiki watakaofika kwa miondoko yake ya taarabu na hasa kibao chake kinachotamba hivi sasa cha mjini chuo kikuu.
Mwendapole amewataka mashabiki kufika kwa wingi kwani hii ni buruda ni ya aina yake ambayo itakuwa na vionjo vya kila aina, na kila atakayefika atafurahi kwani makundi yote haya yatatumbuiza kwa utaratibu maalum ili kila mmoja atii kiu yake.
Kuhusu ulinzi na usalama, amesema yote hayo yameimarishwa
Post a Comment