Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, February 27, 2013

CHELSEA YAIFUNGA MIDDLESBROUGH 2-0 SASA KUKUTANA NA MAN UNITED KWENYE ROBO FAINALI OLD TRAFFORD


JANA usiku Chelsea Wakiwa ugenini kwenye uwanja wa Riverside Middlesbrough katika Mechi ya Raundi ya 5 na Middlesbrough wameifunga bao 2-0. Kipindi cha kwanza kilimalizika bila timu yoyote kuziona nyavu za mwenzake, Dakika ya 51 Ramires akaachia mkwaju ambao umempitia Torres ambaye hakujua haraka kuwa mpira huo umetokomea nyavuni na Ramires kushangilia bao hilo ambalo hata mimi nilijua Ramires pekee ndiye kafunga kumbe ndivyo sivyo!.

Bao la pili likafungwa na Victor Moses dakika ya 73 kwa kazi nzuri ya Hazard na Oscar kuwakaanga mabeki wa Boro kwenye eneo la kipa.


Sasa Chelsea atatua Old Trafford kwenye Mechi ya Robo Fainali kucheza na Manchester United hapo Machi 10.

Fernando Torres akifunga kwa kupitiwa na shuti kutoka kwa Ramires, kumbuka mpira huo umemkuta njiani Torres

Victor Moses akifunga goli baada ya kazi nzuri ya Oscar na Eden Hazard

Ramires akimkumbatia Torres na huku wachezaji wa Chelsea wakifurahia ushindi huo wa bao la pili.

Kocha wa muda wa Chelsea akichachama kuona Chelsea wanawachelewesha kuwafunga Boro
VIKOSI:
Middlesbrough: Steele, Bailey, McManus, Bikey (Hines 35), Friend, Carayol (Zemmama 74), Leadbitter, Rhys Williams, Haroun, Main (Miller 62), McDonald.
Subs not used: Leutwiler, Emnes, Ledesma, Smallwood.
Booked: McManus, Bailey.
Chelsea: Cech, Ferreira, Ivanovic, Terry, Bertrand, Ake, Ramires, Moses (Luiz 76), Oscar (Marin 79), Benayoun (Hazard 58), Torres.
Subs not used: Turnbull, Cole, Lampard, Ba.
Goals: Torres 51, Moses 73.
Ref: Martin Atkinson

RATIBA/MATOKEO
Jumatano Februari 27
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Middlesbrough 0 v Chelsea 2

ROBO FAINALI
Jumamosi Machi 9
[SAA 9 Dak 45 Mchana]
Everton v Wigan Athletic
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Manchester City v Barnsley
Jumapili Machi 10
[SAA 11 Jioni]
Millwall v Blackburn Rovers
[SAA 1 na Nusu Usiku]
Manchester United v Middlesbrough au Chelsea

MFUMO FA CUP:
MSIMU WA 2012/13

NUSU FAINALI: Jumamosi Aprili 13 na Jumapili Aprili 14
FAINALI: Jumamosi Mei 11

No comments:

Post a Comment