VYOMBO VYA HABARI VYA ULAYA VYASIFU TUME YA UCHUNGUZI YA TANZANIA
Baadhi
ya vyombo vya habari vya kimataifa barani Ulaya vimeeleza kuridhishwa na hatua
ya serikali ya Tanzania ya kuunda tume huru inayoongozwa na Jaji Shabani Ally
Lila kuchunguza kwa kina matukio ya vurugu yaliyotokea wakati na baada ya
uchaguzi mkuu.
Vyombo hivyo
vimeeleza kuwa kuundwa kwa Tume hiyo ni hatua inayolenga kuondoa mijadala ya
kisiasa na kurejesha uchunguzi katika ushahidi, sheria na uwajibikaji.
Miongoni mwa
vyombo hivyo ni gazeti la Indegazette la Ubelgiji na shirika la habari la The
News Agency lenye makao yake Brussels, ambavyo vimeangazia muundo wa Tume hiyo
yenye majaji kutoka Tanzania, Namibia na Uganda.
Vyombo hivyo
vimeeleza kuwa uzoefu mpana wa majaji hao unaweza kusaidia kujenga uaminifu
katika mchakato wa uchunguzi.
Hatua ya Rais
Samia Suluhu Hassan kuunda Tume hiyo imeelezwa kuwa inaonyesha Tanzania iko
tayari kuchunguza yaliyotokea kwa kutumia taasisi, sheria na ushahidi ili
kupata majibu.

Post a Comment