SPIKA AHIMIZA UZALENDO MSIMU WA SABASABA

 


  • Spika wa Bunge Mussa Zungu, amewataka Watanzania kuendelea kununua bidhaa zinazozalishwa nchini kama njia ya kuunga mkono viwanda vya ndani na kuchochea ukuaji wa uchumi.

    Akiongoza mamia ya wananchi, viongozi wa Serikali na wadau mbalimbali katika matembezi ya hisani ya Jubilei ya Dhahabu ya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), yaliyofanyika leo Juni 27, 2026, kutoka Shule ya Polisi hadi Viwanja vya Sabasaba, Zungu amesema ni wakati wa kila Mtanzania kuonesha uzalendo kwa kuunga mkono bidhaa za ndani.

    Aidha, amewataka vijana kuthamini amani na kuepuka kutumika katika vitendo vinavyoweza kuhatarisha mustakabali wao, familia zao na taifa kwa ujumla.

    Akihitimisha matembezi hayo, Zungu amesema yamekuwa mwanzo mzuri wa maadhimisho ya Jubilei ya Dhahabu ya Sabasaba na jukwaa muhimu la kuhamasisha wananchi kuunga mkono bidhaa zinazozalishwa nchini.


No comments