MAKALA: HOTUBA YA RAIS SAMIA URUSI NI USHINDI KIUCHUMI, KIJAMII, NA KIDIPLOMASIA!







Na Beda Msimbe,TBN, aliyekuwa Urusi

IJUMAA Juni 5, 2026 ilikuwa siku ya kihistoria na ya kipekee, wakati Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, alisipomama mbele ya viongozi wa dunia katika Jukwaa la Kimataifa la Uchumi (St. Petersburg International Economic Forum) na hoja nzito zenye mashiko, akibeba sauti ya Watanzania wote na kuweka wazi fursa zinazopatyikana Tanzania ikiwa na pamoja na mwelekeo mpya wa nchi katika kutengeneza uchumi wa kisasa.

Jukwaa hilo lilikuwa sehemu muhimu ya ziara ya Rais Samia ambayo haikuwa tu ya itifaki, bali ya kueleza milango wazi ya fursa za kiuchumi na kijamii.

Jinsi Rais Samia alivyopokewa na kukirimiwa nchini Urusi katika shughuli zoye zilizomhusu, ilionesha taswira ya urafiki wa dhati na cheko tupu kati yake na mwenyeji wake, Rais Vladimir Putin. Ziara hiyo ilirudisha historia, ikaweka wazi haja ya sasa baada ya ukombozi wa kisiasa kusaidiana kupatikana kwa ukombozi wa kiuchumi na ustawi wa jamii zote mbili.

Akiwa katika jukwaa la kiuchumi, akizungumza na washiriki hotuba ya Rais Samia iliwatafakarisha wahusika, kwani ilkijaa hoja za uchambuzi wa kina na haja ya dunia kubadilika

Rais Samia alifanya uchokozi wa fikira na moja ya uchokozi huo alisema bila kupepesa kuwa ifikapo mwaka 2050, mtu mmoja kati ya wanne duniani atakuwa Mwafrika; na takwimu hizo kutoka kwa Rais Samia Suluhu Hassan ziliambatana na swali: "Je, Afrika itastawi na kukuaa kwa masharti ya nani, na kwa modeli ya nani ya uchumi?"

Swali hilo lenye mantiki kubwa liliulizwa kwa shauku kubwa kutokana na siasa za kijiopiti ambazo zimekuwa zikiyumbisha ushirika wa kawaida na kujazwa na masharti ya kuangushana na kudhibitiana katika mfumo ambao unamlazimisha maskini asiendelee au kuchaguliwa patna wa kuzungumza naye.

Katika misingi mikubwa ya kufikiri kilojiki Rais Samia alikuwa anaitafadhalisha dunia sio kuistiri Afrika bali kutambua ukweli na kuiacha Afrika ijiamulie mambo yake yenyewe.

Mathalani Afrika kwa sasa ina Ajenda 2063 na soko la AfCFTA, lakini kuna mataifa yanayoendelea kuingilia kati kila mara na kuwatenganisha waafrika ili wajifikirie wanahitaji masaada katika utatuzi wa kero zinazowakabili.

Rais Putin aliunga mkono hoja hiyo, jambo lililoleta miguno ya ridhaa na vigelegele ukumbini.Kuna mambo mengi yanayopaswa kufanywa na Waafrika wenyewe yenye manufaa makubwa kwa binadamu

Mambo yaliyoguswa

Katika hotuba yake na ziara hiyoik ya Urusi Rais Samia amegusa mambo mengi. Hapa tunaweza kuangazia maeneo makubwa yaliyoguswa na jinsi makubaliano yalivyomalizika ikiwa ni mafanikio makubwa kwa Tanzania.

Ikumbukwe kwamba ndani ya ziara ya Rais Samia ambapo pia aliambatana na wafanyabiashara inakumbusha ulimwengu kuhusu mizizi imara ya kidiplomasia kati ya Tanzania na Urusi. Kuna historia ndefu ya mahusiano kuanzia miaka ya uhuru,kwani siku mbili baada ya Tanzania bara kupata uhuru, Urusi ilituma salamu vivyo hivyo kwenye mapinduzi matukufu ya Zanzibar.

Mbele ya wawekezaji, Rais Samia alibainisha kuwa uchumi wa Tanzania unakua kwa kasi ya takribani 6%, ukiwa miongoni mwa chumi zinazochangamka zaidi Afrika.

Alitangaza Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, inayolenga kumfikisha kila Mtanzania kwenye kipato cha wastani cha dola $7,000$ huku akielezea fursa za uwekezaji na biashara nchini Tanzania

Hotuba yake hiyo iliyopigiwa makofi mara kwa mara iliwavutia matajiri wa Kirusi, ambapo sekta binafsi ya Urusi ilikiri kuwa Tanzania ni soko salama na lenye utulivu wa kisiasa unaoruhusu ukuaji wa mitaji.

Lakini hayo yamesemwa wakati pia Rais akieleza kuwapo kwa Mapinduzi makubwa ya Miundombinu (Reli na Bandari). Rais Samia ambaye katika mkutano huo pamoja na ule wa pembeni ambapo wafanyabiashara wa Tanzania walipata nafasi ya kuzungumza na wenzao wa Urusi, alieleza kwa kina ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) inayounganisha Bandari ya Dar es Salaam na nchi za Rwanda, Burundi, na DRC na faida yake kwa wakazi wa eneo hili.

Pia alitaja mpango wa miaka mitano (2026–2031) wa kupanua reli hiyo hadi Musoma, na kuunganisha ukanda wa kusini kuelekea Malawi na Msumbiji. Urusi ikiwa na uzoefu mkubwa wa teknolojia ya reli na usafirishaji, ilionesha nia ya kutoa utaalamu wa kihandisi na mitambo ili kuharakisha uunganishaji wa reli hizo za kikanda.

Suala la kuwepo kwa maboresho ya uwekezaji na mifumo ya saa 24 kulileta msisimko mkubwa. Rais alieleza jinsi uwekezaji ulivyopaa kutoka dola bilioni 3 (2021) hadi dola bilioni 12 (2025) kutokana na mfumo wa usajili wa kampuni unaochukua hadi saa 24 tu. Ni kutokana na kutambulika kwa ukweli huu Taasisi za uwekezaji za Tanzania (TIC) na zile za Urusi zilisaini mikataba ya ushirikiano. Hatua hii ilifungwa kwa cheko na bashasha, kwani urasimu sasa umepigwa marufuku rasmi.

Aidha Miradi ya Eneo Maalum la Kiuchumi la Bagamoyo na Bandari ya Kimataifa ya Mizigo ya Mangapwani (Zanzibar) ilipewa kipaumbele cha juu na makampuni makubwa ya Urusi yanayohusika na masuala ya meli na usafirishaji wa baharini. Wao walikubali kutuma timu za wataalamu nchini Tanzania kufanya upembuzi yakinifu wa namna ya kuwekeza kwenye bandari hizo.

Kwenye Sekta ya Madini Rais Samia alizungumzia haja ya Tanzania ambayo ni Kuongeza Thamani Ndani ya Nchi.Tanzania ikiwa na utajiri wa dhahabu, uranium, nickel, graphite, helium, na madini adimu.

"Hatutaki tena kuuza malighafi pekee, tunataka viwanda vya usindikaji hapa nchini."alisema Rais Samia. Urusi, ikiwa ni mbabe wa madini, ilimalizia haja ya Tanzania kwa kukubali kujenga viwanda (Industrial Parks) nchini Tanzania ili kuchenjua na kuongeza thamani ya madini kabla hayajasafirishwa kwenda nje.

Katikia ziara hii Rais Samia alielezea na kudhihirisha ni kwa namna gani Tanzania iko tayari kwa biashara, ubunifu, na ushirikiano wa kufanikisha kila hatua itakayochangia ustawi wa wananchi wake.

Wakati Rais Samia akimaliza hotuba yake kwenye jukwaa hilo la St Petersburg kwa kutoa shukrani za dhati kwa Rais Vladimir Putin kwa ukarimu wake, viongozi hao wawili walionesha tabasamu la furaha, ikiwa ni ishara ya kukubalika kwa hoja za Tanzania na mwanzo mpya wa dhahabu katika uhusiano wa mataifa haya mawili.

No comments