FURSA ZA AJIRA ZAMWAGWA MIRADI YA MELI ZIWA TANGANYIKA
Ufunguzi wa fursa
mpya za kiuchumi katika mikoa ya pembezoni mwa Ziwa Tanganyika sasa umepata
msukumo mpya baada ya Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA)
kuruhusu uwekezaji mkubwa wa ujenzi wa meli nne za mizigo katika Bandari ya
Karema.
Mradi huu
unaotekelezwa na kampuni ya Gold Voyage Logistics kutoka China, umeanza kuleta
matumaini kwa wananchi wa Rukwa, Katavi, na Kigoma kwa kuzalisha ajira za moja
kwa moja na zisizo za moja kwa moja ambapo kila meli moja inahitaji angalau
mabaharia 15.
Akizungumza na
waandishi wa habari, South Port mkoani Mwanza alisema pia serikali imewekeza Shilingi
bilioni 158.27 katika ujenzi wa meli nyingine mpya ya mizigo Ziwa Tanganyika
itakayoweza kubeba tani 3,500 au mabehewa 25 ya reli ya kisasa ya SGR. Meli hii
itapunguza muda wa safari kutoka Kigoma hadi Kalemie nchini DRC kuwa saa sita
tu.
Msemaji Mkuu wa
Serikali, Gerson Msigwa, akizungumza na waandishi wa habari mjini Mwanza ameeleza
kuwa ujenzi wa meli nne za Karema ulioanza Aprili 2025 umefikia asilimia 95 na
unatarajiwa kukamilika Julai 2026.
Meli hizo zitakuwa na
uwezo wa kubeba kati ya tani 8,000 hadi 10,000 za mizigo kwa wakati mmoja.
Aidha, ukarabati wa
meli kongwe ya MV Liemba kwa gharama ya dola za Marekani 13,192,850 sawa na Shilingi
bilioni 32.9 unaendelea vyema ukiwa umefikia asilimia 55.
Uwekezaji mwingine mkubwa ni mikataba yenye
thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 625 iliyosainiwa na kampuni ya Dearsan
Shipyard ya Uturuki kwa ajili ya ujenzi wa meli mpya mbili na kiwanda cha
kujenga meli.
Juhudi hizi ni
ushadidi wa namna serikali inavyotumia rasilimali fedha kuboresha maisha ya
wananchi na kukuza uchumi wa kikanda kupitia sekta ya uchukuzi.
Post a Comment