RAIS SAMIA AWAAPISHA KABUDI, MAKONDA NA KATAMBI; ATOA MAELEKEZO MAZITO AFCON 2027
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Januari 13, 2026, amewaapisha viongozi mbalimbali aliowateua hivi karibuni katika hafla iliyofanyika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma
Katika hafla hiyo, Rais Samia amefafanua kuwa uteuzi wa viongozi hao umezingatia uwezo, uzoefu, uadilifu, na rekodi zao nzuri katika utumishi wa umma
Maelekezo kwa Mawaziri Wapya
Rais ametoa maelekezo mahsusi kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda, akimtaka kusimamia kikamilifu maandalizi ya Mashindano ya AFCON 2027 ambayo Tanzania ni mwenyeji
Kwa upande wa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Patrobas Katambi, Rais Samia amemtaka kuimarisha amani, utulivu, na kulinda misingi ya haki na utawala wa sheria ili kuongeza imani ya wananchi kwa Serikali

Post a Comment