Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, May 9, 2015

YANGA YAMUUZA MSUVA BILIONI MO

Winga wa Yanga, Simon Msuva.
Na Wilbert Molandi
Dar es SalaamWINGA wa Yanga, Simon Msuva anaendelea vizuri na majaribio katika kikosi cha Bidvest Wits ya Afrika Kusini, uongozi wa timu yake umesema kama akifuzu upo tayari kumuuza kwa dau la dola 700,000 (zaidi ya Sh Bilioni 1.3).

Yanga imeamua kukata mzizi wa fitina baada ya Msuva kutoroshwa katikati ya wiki hii kwenda Afrika Kusini kufanya majaribio katika klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu Afrika Kusini (PSL).
Msuva ambaye mkataba wake unafikia tamati msimu ujao, leo anamaliza majaribio na kurejea nchini usiku na kama akifuzu atakuwa ameitajirisha klabu yake ambayo tayari imetwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara ambapo leo inakamilisha ratiba kwa kucheza na Ndanda FC kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara.

Winga huyo aliyesajiliwa na Yanga misimu miwili iliyopita akitokea Moro United, sasa anasubiri tuzo yake ya ufungaji bora kwani hadi sasa amefunga mabao 17 akifuatiwa na Amissi Tambwe aliyefunga 17. Hata hivyo, Tambwe anaweza kuongeza mengine leo katika mchezo dhidi ya Ndanda.
Kama Msuva akifanikiwa katika majaribio yake anaweza kumtoa kikosini Christopher Katongo raia wa Zambia au Fikru Tefera wa Ethiopia ambao wanaichezea timu hiyo inayomilikiwa na Idara ya Michezo ya Chuo Kikuu cha Bidvets maarufu kama Wits.
Katibu Mkuu wa Yanga, Dk. Jonas Tiboroha, alilihakikishia Championi Jumamosi kuwa, kila mchezaji wa kikosi hicho ana thamani yake lakini wenye viwango vya wastani ni dola 500,000 (Sh milioni 965) na wenye uwezo wa juu ni dola 700,000.
Hiyo ina maana, Msuva ambaye yupo katika kundi la wachezaji wenye viwango vya juu kikosini kwa sasa ana thamani ya dola 700,000.

“Hatumzuii mchezaji kwenda kuichezea timu nyingine, lakini lazima klabu inayomuhitaji ifuate utaratibu ili tupate haki zetu, mchezaji mwenye kiwango cha wastani tunamuuza kwa dola 500,000 na yule mwenye kiwango cha juu ni dola 700,000,” alisema Tiboroha.
“Pia tuna kigezo kingine ambacho tutakitazama kwamba ni lazima timu inayomnunua mchezaji wetu iwe inashiriki michuano ya kimataifa, maana fedha si kila kwetu.”
Endapo Msuva atafanikiwa kujiunga na Bidvest, atakuwa mchezaji wa pili wa kutegemewa na Yanga aliyeshiriki kikamilifu kuipa ubingwa msimu huu kuondoka kwani wa kwanza ni Mrisho Ngassa anayetimkia Free State Stars ya Afrika Kusini pia.

No comments:

Post a Comment