Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, May 9, 2015

YAYA TOURE KUONDOKA ETIHAD 90%

WAKALA wa kiungo Yaya Toure amedai kuwa ana uhakika wa asilimia tisini kuwa mteja wake huyo ataondoka katika majira ya kiangazi. Aprili, Toure ambaye amebakisha mkataba wa miaka miwili ambao unamuingizia kitita cha euro 265,000 kwa wiki, alikuwa akitaka kufanya mazungumzo na maofisa wa City kuhusiana uhamisho katika majira ya kiangazi. Meneja wa Inter Milan, Roberto Mancini ameonyesha nia ya wazi ya kutaka kumsajili kiungo huyo ambaye anatimiza miaka 32 Mei 13, na wakala wake Dimitri Seluk amekiri kuna uwezekano mkubwa wa kuondoka City. Seluk amesema ingawa hakuna kilichoamuliwa mpaka sasa lakini ana uhakika wa asilimia 90 kuwa mteja wake anaweza kuondoka katika timu hiyo majira ya kiangazi. Toure alijiunga na City akitokea Barcelona mwaka 2010 na amefanikiwa kushinda mataji mawili ya Ligi Kuu na moja la Kombe la FA, pia taji la Mataifa ya Afrika akiwa na timu yake ya taifa ya Iviry Coast mapema mwaka huu.Inasemekana wenda akamfuata Robert Mancini Italia

No comments:

Post a Comment