Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, August 22, 2013

CHELSEA YAIFUNGA ASTON VILLA 2-1, WAPANDA KILELENI BAADA YA KUIFUNGA VILLA


Chelsea 2-1 Aston VillaChelsea na Aston Villa wakicheza mchezo wao wa pili kwenye ligi kuu England, Chelsea wakiongozwa na Jose Mourinho wameifunga Aston Villa bao 2-1 ambayo msimu uliopita walikuwa wameinyuka bao 8-0, Mchezo huu ukiongozwa na refa Kevin Friend kwenye uwanja wa Stamford Bridge, jijini London, Blues ndiyo waliotangulia kupata bao la mapema dakika ya 6 kupitia mchezaji Luna bao la kujifunga wao wenyewe. Aston Villa wao wamesawazisha bao dakika za lala salama za kipindi cha kwanza kupitia mchezaji wao C.Benteke dakika za nyongeza za kipindi cha kwanza cha dakika 45.

Dakika ya 73 Ivanovic akaipachikia bao la ushindi la pili na kufanya 2-1 dhidi ya Aston Villa, Dakika za lala salama kipindi cha pili mchezaji John Terry ameunawa mpira na refa kuamua kuukaushia baada ya Terry kuruka juu eneo la hatari la penati na kuupiga mpira kwa mkono.

Ushindi huu unawapandisha Chelsea nafasi ya kwanza na Aston Villa nafasi ya 5 wakiwa na alama 3 wao Chelsea wakiwa na alama 6.
Antonio Luna akiwapachikia bao la kwanza Chelsea Wachezaji wa Chelsea wakipongezanaMchezaji wa Chelsea Ramires na  Fabian Delph wa Villa wakichuana vikali hapaChristian Benteke  akiisawazishia Villa bao na kufanya 1-1 kwenye dakika za majeruhi kipindi cha kwanzaBenteke akishangilia kwa kuruka juu baada ya kufunga bao la kusawazisha dakika chake kumalizika kipindi cha kwanza.Paul Lambert and Jose Mourinho clash
VIKOSI:
Chelsea XI: Cech; Ivanovic, Cahill, Terry, Cole; Ramires, Lampard; Mata, Oscar, Hazard; Ba
Aston Villa XI: Guzan; Lowton, Vlaar, Clark, Luna; El Ahmadi, Westwood, Delph; Weimann, Benteke, Agbonlahor



LIGI KUU ENGLAND
RATIBA
Jumamosi 24 Agosti
14:45 Fulham v Arsenal
17:00 Everton v West Bromwich Albion
17:00 Hull City v Norwich City
17:00 Newcastle United vWest Ham United
17:00 Southampton v Sunderland
17:00 Stoke City v Crystal Palace
19:30 Aston Villa v Liverpool
Jumapili 25 Agosti
18:00 Cardiff City v Manchester City
18:00 Tottenham Hotspur v Swansea City
Jumatatu 26 Agosti
22:00 Manchester United v Chelsea

No comments:

Post a Comment