HISTORIA YA KUSISIMUA YA ‘GANGSTER GRANNY’: BIBI WA MIAKA 100 ANAYEMZIMIA MESSI


Pauline Kana, anayefahamika duniani kote kama 'Gangster Granny', ni bibi wa miaka 100 kutoka nchini Marekani ambaye amejipatia umaarufu mkubwa kupitia video za ucheshi anazozitengeneza akishirikiana na mjukuu wake, Ross Smith.

 Mbali na umaarufu wake kwenye mitandao ya kijamii, Pauline amevutia hisia za watu wengi duniani kutokana na mapenzi yake makubwa na ya dhati kwa nahodha wa timu ya taifa ya Argentina, Lionel Messi.

Bibi huyu ameandika historia ya kipekee kwa kuwa mmoja wa watu wachache waliojaliwa kuishi na kushuhudia mashindano yote ya Kombe la Dunia tangu toleo la kwanza lililofanyika mwaka 1930 hadi lile la mwaka 2026.

Katika mashindano ya mwaka huu, alionekana mara kadhaa viwanjani akiwa amevalia jezi ya Argentina na kubeba mabango yaliyoonyesha wazi mapenzi yake makubwa kwa Messi, kitendo kilichowagusa na kuwafurahisha mashabiki wengi wa soka duniani.

Kama ishara ya upendo na kuthamini uaminifu wake wa muda mrefu kwa mchezo wa soka pamoja na mapenzi yake kwa nyota huyo, Lionel Messi aliamua kumzawadia jezi yake rasmi.

Tukio hilo la kupokea zawadi hiyo lilimletea Pauline furaha kubwa na kuwa moja ya matukio yaliyogusa hisia za mamilioni ya mashabiki, huku likionyesha heshima ya juu aliyonayo Messi kwa bibi huyo ambaye ameshuhudia historia nzima ya Kombe la Dunia katika kipindi chake cha kuishi.

 

 

No comments