MSHTUKO MZITO: MC Pilipili, MC wa Taifa, Afariki Dunia Ghafla Dodoma
Tasnia
ya sanaa na burudani nchini Tanzania imeingia katika simanzi kubwa kufuatia
kifo cha ghafla cha mchekeshaji na mshereheshaji maarufu, Emmanuel Mathias,
anayejulikana kwa jina la jukwaani kama MC Pilipili.
MC
Pilipili, ambaye alijipachika jina la utani la 'MC wa Taifa', amefariki
dunia ghafla mchana wa leo, Novemba 16, 2025, jijini Dodoma, ambako
alikuwa amesafiri kwa ajili ya kutekeleza majukumu yake ya ushereheshaji jioni.
Kifo chake kimeacha mshtuko mkubwa kutokana na jinsi alivyokutwa na mauti
ghafla akiwa katika safari ya kikazi.
Taarifa
za msiba huu zimehakikishwa na mamlaka za Hospitali ya General, Dodoma.
Mganga
Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dkt. Ernest Ibenzi, alithibitisha kuupokea
mwili wa marehemu.
"Ni
kweli tumepokea mwili wa mchekeshaji maarufu nchini MC Pilipili. Amefikishwa
hapa hospitalini akiwa tayari amefariki dunia," alisema Dkt. Ibenzi.
MC
Pilipili atakumbukwa kama mmoja wa washereheshaji mahiri na wa kipekee ambaye
aliweka viwango vipya vya taaluma hiyo nchini.
Mafanikio yake
yanaonekana wazi kupitia takwimu zake mwenyewe, ambapo alijinadi kuwa
amesherehesha Harusi zaidi ya 3060 zenye furaha.
Mafanikio
yake hayakuishia jukwaani tu. Alikuwa na ushawishi mkubwa mitandaoni,
akionyesha jinsi vijana wanavyoweza kujiajiri kupitia fani ya sanaa.
Katika mtandao
wake wa kijamii wa Instagram, alikuwa na jumla ya wafuasi (followers) 457K
na alikuwa ameweka jumla ya posti 39,583.
Uwezo
wake wa kuchekesha, kuunganisha watu na kuacha tabasamu kwa maelfu ya watu
katika sherehe mbalimbali, ulimfanya kuwa kielelezo cha vijana waliofanikiwa
kujenga biashara imara kupitia talanta.
Msiba
huu umegusa nyoyo za wadau wengi wa sanaa, ndugu, jamaa, na marafiki, ambao
wanaendelea kutoa pole kwa familia ya marehemu Emmanuel Mathias.
Mungu
ailaze roho ya Marehemu Emmanuel Mathias (MC Pilipili), MC wa Taifa, mahali
pema peponi. Amina.

Post a Comment