Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, November 19, 2017

YANGA YASHINDA 5-0 CHIRWA NAONDOKA NA MPIRA


OBREY Chirwa leo amezidi kudhirisha ubora wake Yanga akiifungia mabao matatu ‘hat trick’  ilipoibuka na ushindi wa 5-0 dhidi ya Mbeya City katika mechi ya Ligi Kuu iliyochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.
Tangu mwanzo wa mchezo, Chirwa alionekana kuisumbua ngome ya City ambapo alikuwa akiwachomoka mabeki wa timu hiyo mara kwa mara.
Chirwa alianza kuing’arisha Yanga katika dakika ya 28 kabla Emmanuel Martin hajafunga bao la pili dakika tatu baadae akitumia vizuri uzembe wa kipa wa City, Fikirini Bakari.
Dakika moja baada ya kuanza kwa kipindi cha pili, Chirwa aliifungia Yanga bao la tatu kwa mkwaju wa penalti iliyotolewa na mwamuzi Athumani Lazi wa Morogoro baada ya Raphael Daudi kuchezewa rafu na kipa wa City, Fikirini akiwa anaelekea kufunga.
Chirwa ambaye ni mchezaji bora wa Oktoba, alifunga bao lake la tatu, likiwa la nne kwa timu yake katika dakika ya 59 baada ya kuunganisha pasi ya Daudi.
Hat trick ya Chirwa ni ya pili kwenye Ligi Kuu msimu huu, ya kwanza ilikuwa ya Emmanuel Okwi wa Simba aliyofunga kwenye mechi ya ufunguzi ya ligi dhidi ya Ruvu Shooting ambapo Simba ilishinda mabao 7-0.
Karamu ya mabao ilihitimishwa katika dakika ya 88 kupitia kwa Emmanuel Martin akiunganisha pasi ya Gadiel Michael na kuujaza mpira wavuni.
Matokeo hayo yanaibakisha Yanga bafasi ileile ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu ikiwa na pointi 20, nyuma ya Azam yenye pointi 22 sawa na Simba inayoongoza msimamo kwa uwiano mzuri wa mabao.

Azam ilicheza na Njombe Mji ugenini Njombe na kushinda bao 1-0 huku Kagera Sugar nayo ikitamba ugenini kwa ndugu zake Mtibwa Sugar kwenye uwanja wa Manungu, Turiani kwa ushindi wa bao 1-0.

No comments:

Post a Comment