Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, November 19, 2017

EPL YAZIDI KUWA TAMU, LIVERPOOL, ARSENAL CHELSEA NA MAN CITY ZAPATA USHINDI

LIGI Kuu England imezidi kushika kasi, baada ya michezo ya jana kushuhudia miamba Arsenal, Liverpool, Chelsea na Manchester City ikipata ushindi katika michezo yao.
Arsenal iliifunga Tottenham mabao 2-0 Uwanja wa Emirates, matokeo yaliyoifanya ifikishe pointi 22 ikiwa ni moja nyuma ya Tottenham yenye pointi 23, lakini ikibaki nafasi yake ya sita pamoja na ushindi huo.
Ushindi huo wa Arsenal dhidi ya Spurs ni kama unahitimisha ubishi baina ya wapinzani hao wa mji mmoja kuwa ni nani mbabe wa London.
Shokdran Mustafi alikuwa wa kwanza kuiandikia Arsenal bao kwa kichwa dakika a 36, akiunganisha mpira wa adhabu ndogo uliopigwa na kiungo Mesut Ozil baada ya Alexis Sanchez kufanyiwa madhambi.
Kisha Alexis Sanchez alipigilia msumali wa moto jeneza la Spurs kwa kuifungia Arsenal bao la pili dakika ya 41 akimalizia kazi nzuri ya mshambuliaji Alexander Lacazette.
Katika mechi hiyo Arsenal ilifanya mabadiliko mawili katika kikosi kilichofungwa mabao 3-1 na Manchester City.
Ilimuanzisha Alexander Lacazette, lakini pia beki Shokdran Mustafi akirejea kutoka majeruhi akicheza badala ya Francis Coquelin, ambaye hata hivyo aliingia kipindi cha pili.
Nayo Spurs ilifanya mabadiliko ya wachezaji watano kwenye timu iliyoibuka na ushindi dhidi ya Crystal Palace, ikiwakaribisha kipa Hugo Lloris, Kieran Trippier, Ben Davies, Dele Alli na Moussa Dembele na Harry Kane.
Katika mechi nyingine Manchester City iliibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Leicester na kuendelea kukaa kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya England ikiwa na pointi 34.
Mabao ya City yalifungwa na mshambuliaji wa kimataifa wa Brazil, Gabriel Jesus dakika ya 45 na lingine likifungwa na kiungo wa kimataifa wa Ubeligiji, Kevin de Bruyne dakika ya 49.
Chelsea nayo ilipata ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya West Browich. Mabao ya Chelsea yalifungwa na Alvaro Morata dakika ya 17, Eden Hazard dakika ya 23 na 62 na Marcos Alonso dakika 38.

Nayo Liverpool ilipata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Southmpton.

No comments:

Post a Comment