Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, November 19, 2017

WACHEZAJI WATANO WA MPIRA WA MEZA WAENDA CHINA KUJINOA NA MADOLA


WACHEZAJI watano wa timu ya Taifa ya Mpira wa Meza wamekwenda nchini China kuweka kambi kwa ajili ya kujiandaa na mashindano ya Jumuiya ya Madola yanayotarajiwa kufanyika nchini Australia, mwakani.
Akizungumza jana Katibu Mkuu wa Chama cha Mpira wa Meza (TTA) Issa Mtalaso alisema wachezaji waliondoka ni watano kati yao wawili ni wanaume.
“Tumepata bahati wachezaji wetu wamepata kambi ya siku 80 nchini China na wanaondoka leo (jana) naamini kambi hii itakuwa chachu ya kufanya vizuri katika mashindano ya Australia,” alisema Mtalaso.
Mtalaso aliwataja wachezaji hao waliondoka kuwa ni Fathiya Hassan, Masoud Mtalaso, Amon Amaniel, Mwanvita Mohamed na Neema Mwaisuila na kocha Ramadhan Othuman ataungana nao baadae kwasababu bado hajapata kibali cha kutoka nje ya nchi.
Naye Katibu Mkuu wa Kamati ya Olyimpiki Tanzania (TOC) Filbert Bayi alisema anaishukuru serikali ya China kwa kuwapa kambi hiyo ambayo pia wamegharamia tiketi za kwenda na kurudi na wataalamu wa kuwafundisha.
“China inafanya vizuri katika Mpira wa Meza hivyo kambi hii itawasaidia wachezaji wetu katika mbinu hivyo naishukuru Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa kuwapatia kambi hiyo,” alisema Bayi

Pia Bayi alisema anatarajia timu ya ngumi za ridhaa itapata kambi nchini Cuba na riadha itapata kambi nchini Ethiopia kwani bado wizara ya michezo inaendelea kuwasiliana na balozi za nchi hizo hapa nchini kupitia kitengo cha diplomasia ya michezo.

No comments:

Post a Comment