Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, November 19, 2017

KINDA LA JKT RUVU, RASHID CHAMBO APATA ULAJI SWEEDEN


KIUNGO mshambuliaji wa JKT Ruvu, Rashid Chambo amefuzu majaribio katika timu ya AFC ya Sweden.
Akizungumza baba mzazi wa Rashidi mzee Mohamed Chambo ambaye ndiye meneja wa mwanae alisema amefurahi kuona mwanae anakwenda kucheza soka la kulipwa.
“Rashid ni mchezaji mwenye kipaji cha soka kuanzia akisoma nchini Uganda hivyo kufuzu kucheza soka la kulipwa anatimiza ndoto yake ambayo amekuwa nayo,” alisema Chambo.
Pia Chambo alisema Rashid anatarajiwa kurejea nchini Novemba 27 na mwakani Januari 7 atarudi Sweeden kuanza maisha ya kucheza soka la kulipwa.
Kinda huyo mwenye miaka 17 ambaye alikuwa anacheza Serengeti Boys iliyofuzu AFCON za Gabon atakuwa anacheza timu ya vijana lakini pia kocha wa AFC ameshauri awe anacheza kikosi cha wakubwa.
AFC ndiyo timu anayofanya majaribio Said Hamis Ndemla pia anacheza Thomas Ulimwengu


No comments:

Post a Comment