Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, March 22, 2013

BONDIA MNAMIBIA NA MBOTSWANA WASHINDWA KUTAMBIANA


Mtazania Onesmo Ngowi katikati akiwa na baadhi ya maofisa

LILE Pambano lililokuwa likisubiriwa kwa hamu na watu wengi wa kumpata Mfalme wa  wa bantam wa kimataifa kati ya mabondia Immenuel Naidjala a.k.a Prince kutoka Namibia na Lesley Sekotswe kutoka Botswana halikuweza kutoa mshindi baada ya matokeo ya majaji wawili kumpa kila mmoja ushindi wana jaji wa tatu kutoa draw.
Pambano hili lilikuwa limeandaliwa na kampuni ya Sunshine Promotions ya bwana Nestor Tobias na lilikuwa na kila aina ya hamasa baada ya mabondia wote wawili kuonyesha ufundi wa kurusha makonde. 
Rais wa IBF kutoka Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati Mtanzania Onesmo Ngowi ambaye alikuwa ndiye msimamizi mkuu wa mpambani huu alitangaza kuwa mabondia wote wawili watakutana tena baada ya kipindi cha mapumziko ya mwezi mmoja ili kuweza kumpata mshindi wa mkanda huo ambaoni watatu kwa umaarufu katika mkanda ya ngumi. 
Mkanda wa kwanza kwa umaarufu ni wa ubingwa wa dunia. Mkanda wa tatu ni wa ubingwa wa mabara na mkanda wa tatu ni wa ubingwa wa kimataifa ambao ndio uliokuwa unagombewa na mabanodia hao. 
Wakazi wengi wa jiji la Windhoek na miji mingine ya jirani pamoja na nchi za jirani walijazana katika hotel ya Windhoek Country Club and Casino kuushuhudia mpambano huo ambao ulikuwa na kila aina ya hamasa.

No comments:

Post a Comment