Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, February 27, 2013

LIBYA KUFANYA UCHAGUZI WA RAIS WA SHIRIKISHO LA SOKA NA NCHI HIYO TANGU 1962

SHIRIKISHO la Soka nchini Libya, FLF Jumatatu limemteua rais wa kwanza toka kuanzishwa kwa shirikisho hilo mwaka 1962.
 
Anouer al-Tachan ndio jina lililoibuka kidedea katika uchaguzi huo ambao ulihudhuriwa na vilabu mbalimbali nchini humo. Katika mfumo wa zamani shirikisho hilo lilikuwa likimilikiwa na familia ya rais wa zamani wa nchi hiyo Muammar Gaddafi haswa watoto wa kiume wa rais huyo Saadi na Mohammed.

Mfumo mpya katika shirikisho hilo hivi sasa una wajumbe wakuchaguliwa wapatao 12 ambao kazi yao kubwa itakuwa kuratibu na kuweka mfumo mzuri wa uongozi katika kipindi cha mwaka mmoja watakachotawala.

Ligi Kuu nchini humo bado haijachezwa toka kuanguka utawala wa zamani mwaka 2011 kutokana na harakati za kuhakikisha usalama unaimarika kwanza kabla ya kuanza.

No comments:

Post a Comment