Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, February 27, 2013

MAPACHA HOSSAM NA IBRAHIM WAPEWA KIBARUA CHA KUINOA MISR LEL MAKASA

KLABU ya Misr Lel Makasa ya nchini Misri imewateua Hossam Hassan na pacha wake Ibrahim kuinoa timu hiyo msimu huu.

Bodi ya klabu hiyo ilikutana na kuamua kumfukuza aliyekuwa kocha wa klabu hiyo Mohammed Abd El Galel baada ya matokeo mabaya ambayo timu hiyo imekuwa ikiyapata katika ligi.

Mwenyekiti wa Makasa Mohammed Abd El Salaam alithibisha uteuzi wa Hossam na Ibrahim kuinoa klabu hiyo ambapo wataanza kibaria hicho mapema wiki ijayo. Abd El Salaam alidai kuwa walianza mazungumzo na ndugu hao wiki iliyopita na kuafikiana na mpango huo na anawaamini wote wawili kama makocha wazuri na wanaweza kuikwamua timu hiyo na kuipeleka mbali.

Mapacha hao ambao ni wachezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Misri walikuwa wakifundisha klabu ya Al Masry wakati maafa ya Port Saied yalipotokea mwaka 2011 na Zamalek katika msimu wa mwaka 2010. Mbali na timu hizo lakini pia waliisaidia timu ya taifa ya Misri kunyakuwa kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 1998 nchini Burnina Faso chini ya Mahmoud Al Gouhary aliyekuwa akikinoa kikosi hicho wakati huo.

No comments:

Post a Comment