Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, January 27, 2013

MECHI YA SIMBA NA AFRICAN LYON YAINGIZA MILIONI 53

 
Mechi namba 92 ya Ligi Kuu ya Vodacom iliyochezwa jana (Januari 27 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa Simba kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 limeingiza sh. 53,756,000.
Watazamaji 9,408 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo iliyochezwa kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 12,499,752.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 8,200,067.80.
Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 6,355,806.33, tiketi sh. 3,183,890, gharama za mechi sh. 3,813,483.80, Kamati ya Ligi sh. 3,813,483.80, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 1,906,741.90 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,483,021.48.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

No comments:

Post a Comment