Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, September 12, 2023

BONDIA WATATU WAFUZU ROBO FAINALI, DAKAR SENEGAL

Bondia Abdallah Abdallah 'Katoto'


Bondia machachari Abdallah Abdallah 'KATOTO'  amefanikiwa kushinda kwa kishindo dhidi ya mpinzani wake Abdallah Saied Nasser EMAM kutoka Misri kwa points za majaji wote watano (5-0) katika uzani wa 51kg ya bout no. 114.

Sasa jumla ya Watanzania watatu wametinga hatua za robo fainali akiwepo Yusuf Changalawe, Grace Mwakamele na Katoto.

Bondia mwingine wa Tanzania aliyecheza jana awali Musa Maregesi alipoteza kwa pointi dhidi ya mwenyeji kutoka Senegal Kebe Karamba katika uzani wa 92kg ya bout.l no 99.

Leo ni  mapumziko katika michezo hii ya kuwania nafasi za kufuzu kushiriki Olimpiki ya Paris 2024 inayoendelea Dakar, Senegal.

No comments:

Post a Comment