Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, August 1, 2016

MANCHESTER CITY WAMKODELEA MACHO LEROY SANE WA SCHALKE


Leroy Sane anakaribia kumaliza uhamisho wake katika klabu ya Manchester City kutoka Schalke kwa kitita cha pauni milioni 37.

Klabu hiyo ya Bundesliga ilitangaza siku ya Jumatatu kwamba kiungo huyo wa kati hakujiunga na City wakati wa mazoezi yao huko Austria kabla ya kuanza kwa msimu ujao na kwamba alisalia Manchester.

Mkufunzi wa klabu ya Man City Pep Guardiola alithibitisha mnamo tarehe 21 mwezi Julai kwamba alitaka kumsajili Sane.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 aliisaidia Ujerumani kufika nusu fainali za Euro2016,baada ya kucheza mechi yake ya kwanza ya kimataifa mnamo mwezi Novemba.

Alimwambia kkurugenzi wa michezo katika klabu hiyo Christian Heidel kwamba alitaka kuondoka katika klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment