![](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2015/08/08/21/2B3634FC00000578-3190659-image-m-53_1439064360662.jpg)
![](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2015/08/08/20/2B361A9700000578-0-image-a-27_1439062807168.jpg)
Jumamosi iliyopita, Uwanjani Stamford Bridge, katika Dakika za Majeruhi huku Gemu na Swansea ikiwa 2-2 na Chelsea kuwa Mtu 10 baada ya Kipa wao Thibaut Courtois kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu, Fowadi wa Chelsea Eden Hazard alianguka chini kwa maumivu na Refa kuashiria Benchi la Chelsea na ndipo Dokta Eva Carneiro akachomoka mbio kuingia Uwanjani kama kawaida yake kwenda kutoa huduma.
Kitendo hicho kilimkera mno Mourinho na waziwazi alinaswa akimbatukia Dokta Eva Carneiro ambae nae alijibu mapigo.
![](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2015/08/08/21/2B36350000000578-3190659-image-a-38_1439064195076.jpg)
Mourinho alidai Eva Carneiro hajui kusoma Mchezo.
Lakini, katika kile kinachodaiwa kumkandya Mourinho hadharani, Dokta Eva Carneiro aliposti kwenye kurasa yake ya facebook maneno haya: “Napenda kuwashukuru Watu wote kwa sapoti yao. Natoa shukrani kubwa.”
![](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2015/08/08/20/2B360F9600000578-0-image-a-29_1439063004053.jpg)
![](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2015/08/11/17/2B3E0AF000000578-3193920-The_Chelsea_doctor_tends_to_be_private_but_she_posted_on_Faceboo-a-69_1439310231578.jpg)
No comments:
Post a Comment