Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, October 10, 2014

Diego Costa anasema yuko fiti



Diego Costa ameonyesha kutosumbuliwa na tatizo lolote la maumivu ya misuli ya paja baada ya kuanza mazoezi na timu ya Hispania kwa mafanikio ya kujiandaa na michezo ya kufuzu kwa Euro 2016 dhidi ya Slovakia na Luxembourg.
Msambuliaji huyo wa Chelsea amejiunga na mchezaji mwenzake Cesi Fabregas wanaotoka klabu moja, pamoja na nyota wengine wanoacheza ligi soka England akiwemo David Silva na golikipa David de Gea wa Manchester.
Timu hiyo inayofundishwa na kocha mkongwe Vicente del Bosque, iliitandika Macedonia goli 5-1 katika mchezo wa ufunguzi wa michuano hiyo, na sasa ni zamu ya Slovakia pamoja na Luxembourg.
Costa, amefunga magoli tisa katika mechi saba za ligi kuu soka England, akichezea klabu yake ya Chelsea msimu huu, lakini amekuwa na wakati mgumu kupachika magoli akiwa na kikosi cha Hispania katika michezo ya kimataifa hivyo ni wakati mwingine wa mchezaji huyo kuonyesha makali yake katika michezo hiyo miwili ya juma hili.
Wakati huo huo Kocha Del Bosque, amesema kuwa hashangazwi na timu yake kushindwa kuonyesha kiwango cha hali ya juu katika michuano ya kombe la dunia huko Brazil, na kuongeza kuwa timu hiyo iko katika kipindi cha mpito licha ya kupoteza muelekeo katika michuano hiyo mikubwa.
Hata hivyo amewataka wachezaji wake kusahau yaliyopita huko Brazil, kwani hivi sasa ana damu mpya ambazo zina ari ya kutaka kufanya makubwa, ni bora wakawaza mwanzo mpya.

No comments:

Post a Comment