Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, January 8, 2014

KWA MARA YA KWANZA QATAR KUANDAA KOMBE LA DUNIA 2022 KATIKA MAJIRA YA BARIDI.

 KATIBU mkuu wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Jerome Valcke amedai kuwa michuano ya Kombe la Dunia itakayofanyika nchini Qatar 2022 haitafanyika mwezi Juni na Julai kama ilivyozoeleka badala yake itafanyika majira ya baridi. Kumekuwa na mijadala mikubwa toka Qatar walipopewa uenyeji wa kuandaa michuano hiyo Desemba mwaka 2010 kutokana na hofu ya joto kali katika majira ya kiangazi katika ukanda huo ambalo linaweza kuwa hatari kwa wachezaji na mashabiki watakaohudhuria. Akihojiwa na Radio France, Valcke amesema badala ya kufanyika kipindi hicho michuano hiyo inaweza kusogezwa mbele ya kati ya Novemba 15 na Januari 15. Valcke aliendelea kudai kuwa kama michuano hiyo ikichezwa kati ya Novemba 15 na kumalizika Desemba muda huo hali ya hewa itakuwa nzuri tofauti na Juni na Julai.

Modern design: The Al Wakrah Stadium is proposed to be a 40,000-seater venue

Grand designs: The proposed Al-Rayyan football stadium in Doha, to be built for the 2022 World Cup


Spectacular: The Qatar University Stadium in Doha, another one of the proposed venues

No comments:

Post a Comment