Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, January 10, 2014

.............. KUTOA TUZO ZA MAKOCHA TANZANIA

TUZO ya makocha wa mpira wa miguu Tanzania ‘Tanzania Football Coaches Awards 2014’ inatarajiwa kutolewa mapema mwezi machi, mwaka huu, jijini Dar es Salaam.
Akizungumza ofisa mtendaji wa tuzo hizo, Fredrick Luunga alisema lengo hasa ni kuthamini mchango wa makocha wazawa na wa kigeni katika kuendeleza mchezo wa soka hapa nchini.
Luunga alisema kwa miaka mingi, makocha wamekuwa wakifanya kazi hiyo katika mazingira magumu na wamekuwa hawathaminiwi vya kutosha kutokana na mchango wanaoutoa katika kupigania maendeleo ya mchezo huo.
Alisema, anaamini tuzo hiyo itakayokuwa ikitolewa kila mwaka, itasaidia kuibua ari mpya na kuwaongezea morali ya kufanya kazi makocha.

“Hii tuzo kwa makocha wa mpira wa miguu ni ya kwanza kutolewa hapa nchini licha ya kuwepo kwa aina mbalimbali ya tuzo, nafikiri hii itakuwa chachu kwa makocha na wadau wengine”, alisema.
Luunga alizitaja baadhi ya tuzo hizo kuwa ni kocha bora wa mwaka, kocha wa makipa, kocha mkongwe mwenye mafanikio zaidi, kocha bora chipukizi, kocha bora wa kike, kocha bora wa kigeni, kocha wa kigeni aliyewahi kupata mafanikio makubwa alipokuwa akifundisha soka Tanzania na kocha bora mtanzania anayefundisha nje ya nchi.

No comments:

Post a Comment