Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, July 24, 2014

JEREMY MATHIEU ASAJILIWA NA KLABU YA BARCELONA

Barcelona wamemsaini Beki wa Valencia Jeremy Mathieu kwa Mkataba wa Miaka Minne kwa Ada ya Euro Milioni 20.
Mathieu, mwenye Miaka 30, ameichezea France mara mbili na anaweza kucheza kama Fulbeki wa Kushoto au Sentahafu.
Beki huyo anarithi nafasi ya Nahodha wa zamani wa Barcelona Carlos Puyol ambae amestaafu baada ya kuitumikia Klabu kwa Miaka 15. 

Taarifa kutoka Barcelona imesema gharama ya Uhamisho wa Mathieu ni Euro Milioni 20 lakini itabidi pia walipe gharama inayotajwa kwenye Kipingele cha Mkataba wa Mchezaji huyo na Valencia kwamba akiuzwa kabla Mkataba kwisha inabidi ilipwe Euro Milioni 50.
Dau hilo limemfanya Mathieu awe Beki wa umri mkubwa ghali kununuliwa kupita yeyote.
Mathieu aliichezea Valencia Mechi 126 katika Misimu mitano na kufunga Bao 6.
Manchester United imetoa Ofa ya mwisho kwa Juventus ya Pauni Milioni 39 kumnunua Kiungo wao, Juventus, kwa mujibu wa Jarida la Michezo la Italy, Tuttosport.
Ofa hiyo, ya staili ya: 'Chukua Hutaki Basi', inaaminika inaweza kufungua milango kwa Juventus kukubali kumuuza Kiungo wao mahiri kutoka Chile alieng’ara sana huko Brazil kwenye Fainali za Kombe la Dunia. 

Barcelona, ambao walimaliza Msimu uliopita wakiwa Nafasi ya Pili kwenye La Liga, Msimu ujao watakuwa chini ya Kocha mpya Luis Enrique ambae tayari ameshavunja Rekodi kwa kumsaini Straika wa Liverpool, Luis Suarez, kwa Pauni Milioni 75.
Wapya wengine ni Kiungo Ivan Rakitic kutoka Sevill, Kipa Marc-Andre Ter Stegen na Claudio Bravo.
Wachezaji waliohama Nou Camp ni Cesc Fabregas, Puyol, Victor Valdes, Bojan Krkic na Alexis Sanchez.

No comments:

Post a Comment