Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, August 1, 2013

REKODI YA BALE NA MIDINGI MITATU ILIYOTAKA KUMBANIA ISITIMIE

REKODI ya dunia kwenye usajili wa wachezaji imewahi kuvunjwa mara 120 na kwa ujumla wachezaji wote waliowahi kuvunja rekodi ya duniani thamani yao ni pauni 411,964,490 (Sh bilioni 991,202).

Dau hilo linatarajiwa kupanda na kufikiza zaidi ya pauni milioni 500 (Sh trilioni 1.203), kama staa wa Tottenham Hotspur, Gareth Bale ataivunja tena na kuwa mchezaji ghali zaidi duniani akitua Real Madrid.
Kwa mara ya kwanza Sheffield United walivunja rekodi ya usajili mwaka 1913, wakafuatiwa na timu za Preston North End na Derby County, zote mwaka 1949.

Real Madrid wamevunja rekodi ya dunia ya uhamisho mara nne mfululizo, walianza kwa kumsajili Luis Figo, Zinedine Zidane, Kaka na  Cristiano Ronaldo.

Sasa hivi miamba hiyo ya Hispania imeweka mezani dau la pauni milioni 85 (Sh bilioni 204.513) kwa ajili ya kunasa saini ya Gareth Bale.
Ndiyo tunazungumzia kuhusu kuvunja rekodi ya dunia ya uhamisho. Miaka ya nyuma haikuwa fedha nyingi sana, rekodi ya kwanza ya duniani ilikuwa ni pauni milioni 100 (Sh bil 240,604).

Scot Willie Groves alikuwa mchezaji wa kwanza kununuliwa kwa dau la zaidi ya pauni 100, hii ilikuwa alipohama kutoka West Bromwich Albion kwenda Aston Villa kwa ada ya pauni 100 mwaka 1893.
Mwaka 2013 ada hiyo imekuwa mara 800,000 na rekodi kwa sasa bado inashikiliwa na Cristiano Ronaldo, aliyetua Real Madrid kwa ada ya pauni milioni 80 (Sh bilioni 192.483) akitokea Man United mwaka 2009.
Hadi kufikia mwaka huo rekodi ya dunia ilivunjwa mara 41 katika nchi 12 duniani kote.

Diego Maradona amewahi kuvunja rekodi ya dunia ya uhamisho mara mbili mfululizo – mara ya kwanza alipohama kutoka Boca Juniors kwenda Barcelona mwaka 1982 kwa ada ya pauni milioni 3 (Sh bilioni 7.218), miaka miwili baadaye alivunja rekodi yake alipotua Napoli kwa ada ya pauni milioni 5 (Sh bilioni 12.03).

Luis Suarez amewahi kuvunja rekodi hiyo mara moja, siyo Luis Suarez wa Liverpool, huyu ni Suarez wa Hispania ambaye mwaka 1961 alihama kutoka Barcelona kwenda Inter Milan kwa dau la pauni 152,000 (Sh milioni 365.718).  uhamisho wake ndio ulikuwa wa kwanza kuvuka pauni laki moja.
Miaka 14 baadaye uhamisho wa kwanza kuvuka pauni milioni 1 ulifanyika pale staa wa Bologna, Giuseppe Savoldi, alipohamia Napoli kwa ada ya pauni milioni 1.2 (Sh bilioni 2.887)

England walitawala uvunjaji wa rekodi za uhamisho kwenye nusu ya kwanza ya karne ya 20, lakini tangu mwaka 1951, Alan Shearer ndiyo Mwingereza pekee kuvunja rekodi ya dunia ya uhamisho, pale alipohama kutoka Blackburn Rovers kwenda Newcastle kwa ada ya pauni milioni 15 (Sh bilioni 36.09).
Na Manchester United ndiyo timu pekee ya England kuuza mchezaji kwa ada ya rekodi tangu mwaka 1951 pale walipomuuza Ronaldo kwenda Real Madrid mwaka 2009.

Kabla ya mwaka 2000 Real Madrid hawakuwahi kusajili mchezaji kwa ada ya rekodi, lakini tangu mwaka 2000, wamevunja rekodi nne mfululizo za dunia katika usajili wa wachezaji.
Walianza kwa kumsajili Luis Figo kwa pauni milioni 37 (Sh bilioni 89.023), Zinedine Zidane pauni milioni 53 (Sh bilioni 127.52), Kaka pauni milioni 56 (Sh bilioni 134.738) na Ronaldo na wako njiani kuvunja rekodi hiyo kwa mara ya tano mfululizo. Ada ya usajili ya Ronaldo ni kubwa kuliko ada za wachezaji 33 wa kwanza kuvunja rekodi ya dunia zikijumlishwa.

Orodha hii ya kuvunja rekodi ya dunia kwenye usajili ina wachezaji kadhaa wenye majina makubwa kama kina Roberto Baggio, Ruud Gullit, Johan Cruyff, Ronaldo de Lima na Gianluca Vialli.
Sasa hivi Bale yuko njiani kuvunja rekodi ya dunia ya usajili kwa mara nyingine tena na Real Madrid, lakini kuna hii mizee mitatu inayokalia dili hilo la pauni milioni 85.

Joe Lewis
Umri: Miaka 76
Ni nani? Anamiliki hisa nyingi kwenye klabu ya Tottenham Hotspur kupitia kampuni yake ya ENIC.
Utajiri wake: Pauni bilioni 2.6 (Sh trilioni 6.255)
Utajiri wake ameupataje: Ni mtu wa tisa kwa utajiri Uingereza na alipata utajiri wake kwenye biashara ya kubadilisha fedha. Kwa sasa ana kampuni ya Tavistock Group, ambayo ndani yake ipo ENIC, inayomiliki Tottenham.

Nafasi yake kwa Bale: Hana nafasi kwa Bale, anaishi Bahamas, mzaliwa huyo wa London hajihusishi sana na mambo ya wachezaji.
Dili za zamani: Anaendesha klabu yake kupitia kwa Daniel Levy.

Daniel Levy
Umri: Miaka 51
Ni nani? Mwenyekiti wa Spurs na Mkurugenzi Mkuu wa ENIC, Kampuni ya michezo, vyombo vya habari na masuala ya kujiachia inayomiliki klabu ya Tottenham. Mkurugenzi wa zamani wa Rangers.

Nafasi yake kwa Bale: Ukweli usiopingika, Levy amekuwa na tabia ya kuweka ngumu pale linapokuja suala la uhamisho wa wachezaji, mfano sakata la Luka Modric ambaye aliwahi kusema kwamba alihakikishiwa kujiunga Real Madrid, lakini alibaniwa mpaka alipogoma kucheza.

Dili za zamani: Amewahi kufanya dili lukuki za usajili, miongoni mwake ni Michael Carrick (pauni milioni 18 sawa na Sh bilioni 43.308) na Dimitar Berbatov (pauni milioni 30 sawa Sh bilioni 72.181) wote walitua Manchester United. 

Jonathan Barnett
Umri: Miaka 63
Ni nani? Ni Mwenyekiti wa Kampuni ya Stellar Group, hii ni kampuni ya michezo yenye ofisi zake Uingereza, Afrika na Amerika Kusini. Kampuni hiyo inawakilisha wanamichezo 500, tangu mwaka 1994, akishirikiana na David Manasseh. Baadhi ya wachezaji wake ni kama kina Joe Hart, Jack Butland, Scott Sinclair, Kolo Toure na Darren Bent.

Nafasi yake kwa Bale: Ana nafasi kubwa sana kwa Bale, ndiyo wakala wake. Atapata asilimia tano ya 85 kama dili hilo likikubali na angependa kumuona mchezaji wake akiwa Madrid.

Dili za zamani: Alijipatia umaarufu sana kwa kufanikisha uhamisho wa Ashley Cole kutoka Arsenal kwenda Chelsea, uhamisho ambao ulisababisha afungiwe.

No comments:

Post a Comment