Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, December 13, 2012

REDDS' MISS TANZANIA 2012 ZIARANI KAGERA

Redd's Miss Tanzania 2012 Brigitte Alfred, alitua jana mjini Bukoba na  leo tarehe 13 Desemba 2012 ametembelea  Shule maalum ya Mugeza Mseto, inayofundisha wanafunzi wenye ulemavu, pia ametembelea  Kituo cha Nusura ambacho kinatunza watoto yatima kilichopo eneo la  Kashai.
Mrembo Brigitte Alfred, ambaye pia ni Balozi wa Walemavu wa ngozi, [Albinos] ametoa misaada ya kijamii katika vituo hivyo. Vifaa hivyo ni pamoja na Fimbo maalum za kutembelea walemavu wasioona, Miwani, Kofia na Madawa ya ngozi kwa ajili ya Walemavu wa ngozi. Pamoja na vyakula.


Redds Miss Tanzania 2012 pia atatembelea Wilaya ya Misenyi Kesho na kutoa misaada kama hiyo katika kituo kimoja kilichopo wilayani hapa.

Ziara ya Miss Tanzania 2012 imedhaminiwa na Optima Lodge & Safaris pamoja na Victoria Perch Hotel zote za Mkoani Kagera.
Kabla ya kurejea jijini DSM Redds Miss Tanzania 2012 ataelekea Mwanza kwa shughuli zingine za kijamii





No comments:

Post a Comment