SERIKALI YAIMARISHA USHIRIKIANO NA WADAU WA MAHUSIANO



Serikali Kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano  imeendelea kuwafikia wadau wa Mahusiano kwa lengo la kutambulisha Jukumu la Mahusiano na Kupata Maoni kutoka wa wadau hao ili  kuwezesha kuandaa nyaraka mbalimbali za Uimarishaj wa Mahusiano nchini.

Hayo yamebainishwa leo Tarehe 13 Februari 2026 na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu wakati alipotembelea Makao Makuu ya Baraza la Taifa la Mashirika yasiyo ya Kiserikali (NaCoNGO) Mkoani Dodoma.

Alisema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imefungua milango kwa wadau wote wakiwemo mashirika yasiyo ya kiserikali, taasisi za Dini na vyama vya siasa ili kushirikiana katika kujenga taifa lenye mshikamano.



“Tumekutana kujadili namna ya kuimarisha mahusiano na kuendeleza ushirikiano. Mwingi wa utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ni Amani, utulivu na Mshikamano wa kitaifa” Alisema Sangu.

Alisema NaCoNGO imeahidi kuunga mkono juhudi za serikali katika kulinda amani na kusimamia maadili kupitia vyombo vyao vya ndani ili kuhakikisha mashirika wanachama yanafuata Miki na taratibu walizoweka.

Sangu Alibainisha kuwa zaidi ya mashirika 8,000 yaliyo hai chimichanga mchango mkubwa katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya 2050.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Mashirika yasiyo ya Kiserikali Jasper Makala ameishukuru serikali kwa kuiheshimisha sekta hii ya Mashirika yasiyo ya kiserikali. Alisema ziara hiyo imeimarisha mazungumzo na ushirikiano Kati ya serikali na Mashirika yasiyo ya kiserikali.

No comments