Uwekezaji katika Michezo chachu ya maendeleo nchini
WAZIRI
wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amesema
Maendeleo ya michezo yamechangiwa na juhudi kubwa za viongozi wakuu wa nchi Dkt.
Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na Mhe. Dkt.
Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ambao
wameweka vipaumbele katika sekta hiyo.
Amezungumza
hayo Januari 24, 2026 wakati akifunga Mashidano ya mpira wa Pete ya Kombe la
Muungano Zanzibar ambapo timu ya KVZ imeibuka bingwa baada ya kushinda michezo
yote 10.
"Kupitia
mpango wa "Goli la Mama", tumeshuhudia ongezeko la Bajeti, ujenzi wa
viwanja vipya na mazingira bora kwa wanamichezo wetu, matokeo ya jitihada hizi
ni wazi na tumeshuhudia Timu ya Taifa ya mpira wa miguu ‘Taifa stars’ imefika
hadi hatua ya 16 bora ya michuano ya AFCON pale Morocco na ni kwa mara ya
kwanza tangu kuanza kushiriki mashindano hayo," amesema Mhe. Masauni.
Amesema
ujenzi pamoja na uboreshaji wa Viwanja vya michezo vimewezesha mashindano
mbalimbali kufanyika yakiwemo mashindano ya CHAN yaliyohusisha nchi za Kenya,
Uganda na Tanzania. Huu ni ushahidi kuwa Tanzania, kupitia Muungano wake,
inainuka kisoka Afrika na Duniani.
Ameeleza
Maendeleo haya yamewekewa chachu ya ushirikiano kati ya serikali zetu mbili
chini ya wizara husika za michezo na taasisi zetu za ZFF, TFF, CHANEZA NA
CHANETA ambazo zinasimamia michezo hii ya mpira wa miguu na Pete kwa weledi
mkubwa sana.
“Nawapongeza
viongozi wa wizara hizi na wasaidizi wao pamoja na viongozi wa ZFF, TFF,
CHANEZA NA CHANETA kwa kuhakikisha wanasimamia maendeleo ya michezo nchini,"
ameongeza Masauni.
Aidha katika hatua ingine Waziri Masauni amewashukuru waandaji wa Mashindano haya CHANEZA na CHANETA na Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kutekeleza agizo la Rais la kuimarisha Muungano kupitia michezo alilolitoa Aprili 13, 2024 wakati akipokea taarifa ya Kamati Maalum iliyowasilisha maandalizi ya Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwa
upande wake Mwenyekiti wa CHANEZA Bi. Nasra Juma ameishukuru Ofisi ya Makamu wa
Rais kwa kushiriki na kudhamini
mashindano hayo ambayo yamekuwa ya ushindani mkubwa.
Amesema
mashindano hayo ni muhimu kwa kuwa yamekuwa yakitoa wawakilishi wa Tanzania
katika mashindano makubwa kwa Bara la Afrika na jumuiya ya Afrika Mashariki. Mashindano
haya yalishirikisha timu 11, tano kutoka Zanzibar na sita kutoka Tanzania Bara.
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
Post a Comment