Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, July 24, 2024

AZIZI KI, FEI TOTO WAKABANA KOO TUZO ZA TFF

 

Fei Toto

Aziz Ki

TUZO ya mchezaji bora wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2023/2024 imeonekana kuwa na ushindani baada ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kutoa orodha ya wachezaji wanaowania tuzo mbalimbali.

Katika tuzo hizo zitakazotolewa Agosti 1, mwaka huu Masaki, Dar es Salaam kipengele cha mchezaji bora kinawaniwa na wachezaji wanane ambao ni Stephane Aziz Ki, Feisal Salum ‘Fei Toto’, Kipre Jr. Djigui Diarra, Ley Matampi, Yao Kouassi, Ibrahim Bacca na Mohamed Hussein ‘Tshabalala’.

Katika kipengele cha kipa bora wa Ligi Kuu Tanzania Ayoub Lakred, Djigui Diarra na Ley Matampi kwa upande wa mabeki ni Yao, Bacca na Tshabalala, tuzo ya kiungo bora Aziz Ki, Fei Toto na Kipre Jr, kocha bora ni David Ouma, Bruno Ferry na Miguel Gamondi.

Aziz Ki huenda akatwaa tuzo zaidi ya moja kwa sababu tayari tuzo ya mfungaji bora wa Ligi Kuu ni yake kwa kuwa anaongoza kwa kufunga mabao 21.

Pia Fei Toto ana nafasi nzuri ya kuondoka tuzo, kwani alikuwa na msimu bora na alimaliza ligi akishika nafasi ya pili katika ufungaji wa mabao akiweka kambani mabao 19.

Aidha tuzo zilijumuisha mashindano yote yaliyochini ya TFF kuanzia Ligi Kuu zote kwa maana ya wanawake na wanaume, Championship, First League, soka la ufukweni, Kombe la Shirikisho na Ligi ya Vijana ya U20.

Kadhalika kutakuwepo na tuzo ya mchezaji bora anayecheza nje ya nchi wa kiume na wanaowania ni Mbwana Samatta, Himid Mao na Novatus Dismas na kwa wanawake wapo Opa Clement, Clara Luvanga na Aisha Masaka.

No comments:

Post a Comment