Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, September 12, 2023

DK NDUMBARO AMPA KARIA MAUA YAKE WAKISAINI MKATABA NA SANDALAND FASHION WEAR LTD

 




Na Rahel Pallangyo

SERIKALI imepongeza uongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa kuingia mkataba wa miaka mitano na Kampuni ya Sandaland Fashion Wear LTD wenye thamani ya Sh bilioni 3 kwa ajili ya kuzivalisha timu zote za Taifa.

Pongezi hizo zilitolewa na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Damas Ndumbaro, Dar es Salaam juzi baada ya kushuhudia utiaji saini wa mkataba huo.

“Nashukuru sana uongozi wa TFF chini ya uongozi wa ndugu yangu Wallace Karia, ambapo kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi hii, TFF inaingia mkataba na mtengenezaji jezi kwa ajili ya timu zote za Taifa, tunaweza kulichukulia jambo hilo kama dogo sana lakini halijawahi kufanyika na linafanywa na TFF chini ya jemedari Wallace Karia,”

“Nasisitiza haya kwa sababu sisi Watanzania ni wazuri sana wa kukosoa lakini tunakuwa wachoyo kusifia pale jambo zuri linapofanyika na kwa mara ili timu zote za taifa ziwezi kupata jezi rasmi zinazotengenezwa na kampuni yenye heshima kubwa hapa Tanzania,” alisema Dk Ndumabaro.

Naye Rais wa TFF Wallace Karia alisema mkataba huo utahusisha timu zote za Taifa na katika mkataba huo watakuwa wanapewa jezi bure kwa timu zote na watakuwa wanapata fedha.

“Leo tunatimiza ahadi yetu ya kuongeza wadhamini zaidi. Mkataba huu ni wa kihistoria kwani tutakuwa tunapata jezi bure na pia tunapata fedha jambo halijawahi kutokea,” alisema Karia.

Pia Karia alisema huo ni utekekezaji wa maagizo ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kutaka wawekezaji wazawa kupewa nafasi zaidi ambapo alisema atakuwa anawalegezea kwenye kodi.

Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya Sandaland Fashion Wear LTD, Yusuph Yenga alisema kampuni hiyo ina uzoefu wa kutengeneza jezi na kuahidi kuwa jezi hizo zitakuwa na ubora na viwango vya hali ya juu.

Mkurugenzi wa Tume ya Ushindani (FCC), William Erio alipongeza TFF kwa mafanikio waliyopata katika kipindi cha uongozi wa Karia.

“Sisi Tume ya ushindani ni kuhakikisha wafanyabiashara wanafanikiwa kwa kuweka mazingira mazuri na nimefurahi kuona kampuni ya wazawa imeshinda zanuni ya kutengeza jezi za timu za Taifa,”

No comments:

Post a Comment