Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, November 21, 2017

HATUSHINDANI NA SIMBA

KOCHA Msaidizi wa Yanga, Shadrack Nsajigwa amesema hawashindani na Simba bali wanatimiza malengo waliojiwekea tangu kuanza kwa msimu wa ligi kuu.
Kauli hiyo aliitoa juzi baada ya mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliochezwa Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam dhidi ya Mbeya City na kushinda mabao 5-0 jambo ambalo wengi wanasema Yanga imeshinda mabao mengi ili kupunguza gepu la mabao dhidi ya Simba.
“Yanga haishindani na Simba labda Simba ndio inashindana na sisi kwani tumejiwekea malengo tangu msimu unaanza na ndio tunayatimiza,” alisema Nsajigwa
Pia Nsajigwa alisema ushindi huo umetokana na wachezaji kufuata maelekezo ya benchi la ufundi na kucheza vizuri.
Naye kocha wa Mbeya City Nsanzurwimo Ramadhani alikiri timu yake kucheza vibaya na kukubali kubeba lawama zote za kupoteza mchezo huo.
“Timu haikucheza vizuri na tumepoteza mchezo kwa idadi kubwa ya mabao lakini wachezaji wasilaume badala yake lawama hizo nazibeba mimi,” alisema Ramadhan
Pia Ramadhan alisema kuweka kambi sehemu tofauti tofauti haimaanishi kuwa huwezi kufungwa maana kuna timu zinakwenda kuweka kambi nje ya nchi na zinafungwa.
Huu ulikuwa mchezo wa kwanza kwa Mbeya City kufungwa mabao mengi tangu ianze kucheza ligi kuu kwani Yanga iliwahi kuifunga mabao 3-0.

Baada ya kumalizika mzunguko wa kumi Yanga inashika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 20 nyuma Azam FC yenye pointi 22 sawa na vinara Simba na Mbeya City inashika nafasi ya tisa ikiwa na pointi na pointi 11.

No comments:

Post a Comment