Yaliyojiri Jioni ya Futari na Tuzo Simba
Zimbwe pia ndiye mchezaji bora wa ligi kuu ya Vodacom msimu huo baada ya kucheza kwenye kiwango bora huku akifanikiwa kushuka dimbani katika mechi zote msimu mzima. Tayari Wekundu hao wameinasa saini ya beki Jamal Mwambeleko kutoka Mbao FC kwa ajili ya kumsaidia Zimbwe kutokana na kucheza mechi nyingi bila kumpumzika ambapo kwa sasa ni majeruhi.
Katika hafla hiyo mshambuliaji Moses Kitandu nae alikabidhiwa tuzo ya mchezaji bora chipukizi. Kitandu alipandishwa kwenye kikosi cha wakubwa baada ya kuonyesha uwezo mkubwa akiwa na vijana (U20) lakini hata hivyo kocha Joseph Omog hakumpa nafasi kubwa ya kucheza.
Nae mfanyabiashara Mohammed Dewji ‘MO’ amepewa cheti maalum kwa ajili ya kutambua mchango wake kwa timu hiyo katika masuala mbalimbali hasa yanayohusu fedha.
Mohamed Dewji ‘Mo’
Post a Comment