EDEN HAZARD AIPAISHA CHELSEA KILELENI,
Kocha Jose Mourinho
Ushindi huu umewapa Chelsea uongozi wa Pointi 10 mbele ya Timu ya Pili Arsenal na Man United kubaki Nafasi ya 3 wakiwa Pointi 11 nyuma.
Chelsea walifunga Bao lao la ushindi Dakika ya 38 kupitia Eden Hazard baada ya pasi nzuri ya kisigino ya Oscar kwenye Mechi ambayo Man United walimiliki Mpira kwa Asilimia 70 dhidi ya 30 ya Chelsea.
Katika Dakika za mwishoni Refa Mike Dean aliinyima Man United Penati baada ya Ander Herrera kuangushwa ndani ya Boksi na badala yake kumpa Kadi ya Njano.
Chelsea: Courtois, Ivanovic, Terry, Cahill, Azpilicueta, Zouma, Matic, Oscar, Fabregas, Hazard, Drogba.
Akiba: Cech, Luis, Ramires, Mikel, Willian, Cuadrado, Solanke.
Man Utd: De Gea, Valencia, Smalling, McNair, Shaw, Rooney, Mata, Ander Herrera, Fellaini, Young, Falcao.
Akiba: Da Silva, Di Maria, Januzaj, Van Persie, Valdes, Blackett, Pereira.
Refa: Mike Dean.
Post a Comment