Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, February 13, 2014

ARSENAL 0 v MANCHESTER UNITED 0, HAKUNA MBABE!


Mtanange umemalizika punde kwa sare ya 0-0 kwenye uwanja wa Emirates.
Olivier Giroud sends a gilt-edged chance inches wide.Mtanange kati ya Arsenal na Man United umemalizika timu zote mbili zikishindwa kutambiana baada ya kumalizika dakika 90 kwa kutoka sare kwenye uwanja wa Emirates.
Licha ya Arsenal kupata nafasi nyingi za kufunga mipira yote iliishia nje huku Mchezaji wake Giroud kukosa bao za wazi mara mbili. Kwa upande wa United Robin Van Persie nae kakosa mapema kipindi cha kwanza baada ya kuwatoka mabeki wa Arsenal na kubaki na kipa na kuachia shuti na kudakwa na mlinda mlango wa Gunners. 
Sare hii ya 0-0 inawabakisha Arsenal katika nafasi ya pili wakiwa na pointi 56 na wao Man United wakibakia pia pale pale walipokuwa katika nafasi ya 7 wakiwa na pointi 42.Mesut Ozil na Rafael wakigombea mpiraMichael Carrick na Tomas Rosicky wakichuana mapema kipindi cha kwanzaMzee mzima Sir Alex Ferguson alikuwepo kwenye uwanja Emirates Stadium, London. Taswira, Viongozi wa Man UnitedAliyekuwa mchezaji wa Arsenal Robin Van Persie, nusura aifunge klabu yake ya zamani lakini juhudi zake zilizimwa na Wojciech Szczesny.Mchezaji wa Manchester United Chris Smalling akichuana na Olivier GiroudMchezaji wa Manchester United Wayne Rooney na Nemanja Vidic walimzonga mwamuzi Mark Clattenburg, baada ya mwamuzi huyo kuminya Rooney alipoangushwa katika kipindi cha kwanza.Mchezaji wa Manchester United Wayne Rooney akiteta na mwamuzi mkuu Mark Clattenburg kulia!
Arsenal imepoteza nafasi ya kurejea tena kileleni mwa ligi kuu ya Premier, baada ya kutoka sare ya kutofungana bao lolote na Manchester United katika uwanja wao wa nyumbani wa Emirates.
Vijana hao wa Arsene Wenger, walikuwa wakijaribu kufuta aibu waliopata wiki iliyopita wakati walipofungwa magoli 5-1 na Liverpoool nayo Manchester United, kwa upande wake ilikuwa ikijinasua baada ya kutoka sare ya kufungana magoli mawili kwa mawili na Fulham mwishoni mwa juma lililopita.

Licha ya kuwa mechi hiyo ilikosa ladha ya hadhi ya timu mbili kuu zinapocheza, pande hizo mbili zilipoteza nafasi nyingi za kufunga.
Hata hivyo ilibidi timu hizo mbili kugawana alama moja kila moja na Sasa Arsenal imesalia katika nafasi ya pili na alama 56 alama moja tu nyuma ya Chelsea.
Mchezaji wa Arsenal Mesut Ozil na Mchezaji wa Manchester United Robin van Persie kwenye patashika za hapa na pale!Majanga!! Mchezaji wa Arsenal's Olivier Giroud akimtegeshea Mchezaji wa Manchester United Rafael da Silva na kuanguka chini vibaya na kulazimika kutoendelea na kipindi cha pili.Kocha mkuu wa United David Moyes kwenye wasiwasi baada ya kuona mchezaji wake Rafael da Silva kaumiaMchezaji wa Arsenal Jack Wilshere (katikati) akiwapelekesha mtu mbili wa Manchester United Antonio Valencia na Michael Carrick.Mchezaji wa Arsenal Jack Wilshere na Michael Carrick wakipepetana hapa huku Jack akimwekea msosi na kumsukuma ili asiweze kuleta shida kwa mlinda mlango wao.Mchezaji wa Arsenal Kieran Gibbsna Mchezaji wa Manchester United Chris Smalling kwenye patashika, Smalling akijaribu kumzuia Gibb.Jack Wilshere gets kwenye kasi na Tom Cleverley nyuma yake!

RATIBA/MATOKEO
Jumatano Februari 12
Arsenal 0 v Manchester United 0
Everton v Crystal Palace p-p
Man City v Sunderland p-p
Newcastle 0 v Tottenham 4
Stoke City 1 v Swansea 1
Fulham 2 v Liverpool 3

No comments:

Post a Comment