Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Sunday, May 26, 2013

NEYMAR ASAINI MIAKA MITANO BARCELONA, AIPA KISOGO REAL MADRID,

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil atajiunga na Barcelona kwa mkataba wa miaka mitano baada ya kukataa ushawishi wa Real Madrid, ambao wanaamini kwamba walitoa ofa nono ya euro milioni 35.

Mshambuliaji huyo ataingiza malipo binafsi ya euro milioni 7 kwa mwaka, ambayo licha ya kwamba ni pungufu ya ambayo angepata Real Madrid, yatamshuhudia akipata malipo ya ziada kutokana na maafikiano ya mkataba na kampuni ya kimataifa ya vifaa vya michezo ya Nike.
Mabingwa hao wapya wa La Liga, hata hivyo, wamewapiku mahasimu wao Real katika kumsajili Neymar ambaye atajiunga nao katika kipindi hiki cha usajili kujiandaa na msimu ujao wa 2013-14.

Lionel Messi (L) of Spain's Barcelona is greeted by Neymar of Brazil's Santos after their Club World Cup final soccer match in Yokohama, south of Tokyo December 18, 2011. (Photo : REUTERS/Toru Hanai (JAPAN - Tags: SPORT SOCCER) ) 

No comments:

Post a Comment