Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, March 22, 2013

RIO FERDINAND BAADA YA KUJITOA KWENYE KIKOSI CHA UINGEREZA SASA ATAKUWA ANAONEKANA KWENYE RUNINGA KAMA MCHAMBUZI WA SOKA

Rio Ferdinand ambaye alijitoa katika kikosi cha Uingereza kitakacheza mechi ya kufuzu michuano ya Kombe la Dunia kutokana na matatizo ya mgongo yanayomsumbua, anatarajiwa kwenda nchini Qatar kufanya kazi ya uchambuzi katika luninga itakayorusha matangazo ya moja kwa moja ya mechi ya Uingereza dhidi San Marino kesho. Beki huyo anayecheza klabu ya Manchester United amekubali kufanya kazi ya uchambuzi katika luninga ya Al Jazeera kwa ajili ya mchezo wa San Marino pamoja na kwamba itakuwa ni safari ya saa 15 mpaka makao makuu ya kituo hicho yaliyopo Doha. Ratiba hiyo ya safari itamsaidia nyota huyo kutatua tatizo lake la mgongo ambalo lilipelekea kujitoa katika kikosi cha Roy Hodgson. Mara baada ya kutua nchini Qatar mapema leo asubuhi Ferdinand aliandika katika ukurasa wa mtandao wake wa kijamii wa twitter kufurahia safari. Uamuzi wa mchezaji huyo kwenda Qatar unaweza kuwakera mashabiki wa soka wa Uingereza pamoja na Chama cha Soka cha nchi hiyo FA.

Hata hivyo kocha Hodgson akijibu swali kuhusiana na Ferdinand kusafiri hadi Qatar kuchambua mechi ambayo angekuwa uwanjani akicheza,alisema hakuwa na wazo lolote,lakini amejisikia vibaya kuona beki huyo hajajiunga na timu yake na kusafiri kwake kwenda Qatar ni matakwa yake binafsi na klabu yake.

Mechi ya mwisho Ferdinand kuichezea England ilikuwa dhidi ya Uswis mwezi Juni mwaka 2011,Alikosa fainal za mataifa barani Ulaya mwaka 2012 ambapo kocha Roy Hodgson alisema ameacha kumuita nyota huyo kwa sababu za Kimpira.
Hivi sasa Hodgson itamlazimu kumchagua beki wa Manchester City Jeleon Lescott, Chris Smalling wa Manchester United ama Steven Caulker wa Tottenham au Steven Taylor wa Newcastle United kwenye safu ya ulinzi itakayocheza na visiwa vya San Marino Ijumaa hii katika mchezo wa kundi H kusaka tiketi ya kushiriki kombe la dunia mwakani nchini Brazil.


Marathon: This graphic shows Ferdinand's epic trip to Qatar in comparison to the much smaller journey to San Marino for the England squad
Luxury: Ferdinand will stay at the Grand Heritage hotel at the Aspire Academy in Doha, Qatar

 An aerial view of the Aspire Academy that is used by a number of the world's leading football clubs

England's players have been training this week ahead of the World Cup qualifying double-header
Ferdinand is a big fan of the Aspire Academy in Doha - and was part of the United squad who spent their winter break there

HISTORIA YA FERDINAND TIMU YA TAIFA. 
•1997: Alicheza mechi ya kwanza dhidi Cameroon kwenye uwanja wa Wembley
•1998: Alikuwa kikosi kilichoshiriki kombe la dunia.
•2000: Aliachwa kwenye kikosi kilichoshiriki kombe la mataifa ya Ulaya.
•2002: Alifunga bao lake kwanza akiwa katika ushindi wa 3-0 dhidi ya Denmark katika michuano ya kombe la Dunia.
•2004: Alifungiwa miezi nane kwa kushindwa kufanya vipimo vya madawa ya kuongeza nguvu michezoni.
•2006: Alicheza mechi tano za kombe la dunia nchini Ujerumani.
•2008: Alivaa kitambaa cha Unahodha kuiongoza England katika mechi ambayo walipoteza dhidi ya Ufaransa.
•2010: John Terry anavuliwa unahodha na Ferdnand alipewa,lakini kutokana na majeruhi alishindwa kushiriki Michuano ya kombe la dunia.
•2011: Alitimiza mechi yake ya 81 wakati England ilipocheza dhidi ya Uswis katika mechi ya kufuzu kombe la mataifa barani Ulaya.

No comments:

Post a Comment