Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, March 20, 2013

ANTONIO VALENCIA AKIRI KIWANGO KIMESHUKA LAKINI MAN UTD ITAMALIZA MSIMU IKIWA VIZURI

Mchezaji winga wa Manchester United Antonio Valencia amekiri kuwa Msimu huu umemvunja moyo tofauti na Msimu uliopita ambao alitwaa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Msimu ndani ya Klabu yake. 

Msimu huu, Valencia, mwenye Miaka 27, amekuwa hana mtiririko wa Uchezaji safi na kumfanya awe amecheza Mechi 21 za Ligi kati ya 29 zilizochezwa na Man United.
Akiongea na Jarida la Klabu ya Man United liitwalo United Review, Valencia ametamka: “Huu haukuwa Msimu mwema kwangu. Nimepata maumivu na kuna wakati Mguu bado unasumbua. Hilo limeathiri kiwango changu. Lakini natumai ntapata nafasi za kucheza Mechi nyingi zaidi na nitajitahidi kufanya vyema zaidi kwa ajili ya Wachezaji wenzangu, Meneja na Mashabiki.”
Tayari Valencia ameshawahi kutwaa Ubingwa akiwa na Man United na safari hii wako tena njiani kutwaa Ubingwa mwingine wakiwa Pointi 15 mbele ya Timu ya Pili Man City huku Mechi zikiwa zimebaki 9 na miongoni mwa hizo ni dhidi ya Manchester City, Arsenal na Chelsea.

Lakini Valencia amesisitiza ari ya Wachezaji wenzake wanaodhamiria kulirudisha Taji tena Old Trafford baada ya kulikosa Msimu uliopita na kuchukuliwa na Man City waliposhinda Mechi ya mwisho na kufungana Pointi na Man United na wao kuwa Mabingwa kwa tofauti ya Magoli.
Valencia amesisitiza: “Tuna ari na hatutaki kurudia ya Msimu uliopita. Kila Gemu kwetu sasa ni kama Fainali- lazima tupigane kila Dakika ya mchezo. Tunajua Ubingwa uko mikononi mwetu na lazima tuhakikishe tunashinda!”

Frustrated: Antonio Valencia has this season struggled for his usual consistency
Frustrated: Antonio Valencia has this season struggled for his usual consistency
Competition: England frontman Danny Welbeck has this season been used on the right wing
Competition: England frontman Danny Welbeck has this season been used on the right wing
Key performer: But Rio Ferdinand is unavailable for England
Key performer: But Rio Ferdinand is unavailable for England
Tunnel vision: Valencia is concentrated on United's push for honours
Tunnel vision: Valencia is concentrated on United's push for honours

No comments:

Post a Comment